Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Je, vikosi maalum vya Uingereza viliwauwa kinyume cha sheria Waafghani 80 wakiwa wametumwa kupigana na Taliban? Hivi ndivyo uchunguzi ambao unachunguza kipindi cha mwaka 2010-2013 na hatua za jeshi nchini Afghanistan. Kwa nia ya uwazi, tume imechapisha siku ya Jumatano , Januari 8, muhtasari wa mahojiano saba yaliyofanywa na wanajeshi au maafisa waliotumwa wakati huo.

Mapema mwaka wa 2010, wanajeshi kadhaa walielezea wasiwasi wao kwa wakuu wao. Wasiwasi ulirejea kwa hakimu anayesimamia uchunguzi: kulingana na wao, huko Afghanistan, vikosi maalum vya Uingereza viliua watu ili wajisikie tu kuwa waliua. Watoto, wenye umri wa miaka 16 na chini, watu wasio na silaha au watu binafsi wasio na uhusiano na Taliban, walilengwa naa jeshi hilo la Uingereza. Kubwa zaidi, mauaji mengine yalidaiwa kufichwa ili kutoa hisia ya kujihami.
Na katika kambi, askari walijivunia kuwa “wameangamiza” Waafghan au walijaribu kuvunja rekodi za watu waliouawa. Madai haya yanawiana na uchunguzi uliofanywa kwa miaka mingi na BBC kuhusu unyanyasaji wa vikosi maalum nje ya nchi.
Uchunguzi wa kimahakama, ambao kusikilizwa kwake hufanyika kwa siri ili kulinda utambulisho wa mashahidi,utabaini kama jeshi liliwaua kihalali Waafghanistan 80 na kama makao makuu ya jeshi walichukua hatua zinazofaa baada ya kuonywa. Wanachama kadhaa wa kikosi maalum cha Uingereza pia wanashutumiwa kwa mauaji nchini Libya na Syria.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.