Mpinzani wa Cambodia na mbunge wa zamani auawa Bangkok, polisi wa Thailand wanamsaka.

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mbunge wa zamani wa upinzani nchini Cambodia, mwenye asili ya Khmer na Ufaransa, Lim Kimya, ameuawa kwa kupigwa risasi siku ya Jumanne mtaani Bangkok. Polisi wa Thailand wametoa hati ya kukamatwa kwa mtu anayeshukiwa kuhusika na mauaji hayo, kwa sababu zinazochukuliwa kuwa za “kisiasa” na kiongozi wa upinzani wa Cambodia aliye uhamishoni Sam Rainsy.

Mbunge wa zamani wa upinzani Lim Kimya mnamo 2017 wakati wa mahojiano na AFP.
Mbunge wa zamani wa upinzani Lim Kimya mnamo 2017 wakati wa mahojiano na AFP. AFP – TANG CHHIN SOTHY

“Lim Kimya (…) amefariki papo hapo,” Gazeti la Bangkok Post mnamo Jumanne, na kuongeza kwamba “polisi walikuwa wakimtafuta muuaji.” Mwanaume anayetafutwa na vyombo vya sheria ni askari wa zamani wa jeshi la wanamaji la Thailand, vyombo vya habari vya ndani vimeripoti. “Tunachunguzia sababu kwa sasa, hatuna habari nyingi, isipokuwa anafanya kazi kama dereva wa teksi ya pikipiki,” Sanong Sangmanee, mkuu wa polisi katika wilaya ya Bangkok ambako tukio hilo lilitokea.

Lim Kimya ameuawa na mwanamume aliyekuwa kwenye pikipiki siku ya Jumanne alasiri katika wilaya ya kitalii ya Bangkok, ambapo basi kutoka Siem Reap (kaskazini magharibi mwa Kambodia) lilikuwa limemshusha tu, pamoja na mkewe Mfaransa. Picha za uchunguzi wa video zilizoruswa kwenye vyombo vya habari vya Thailand zinaonyesha mshukiwa akiwa amepanda skuta nyekundu, akiwa amevalia suruali ya jeans, na mfuko ukiwa juu ya bega lake.

“Mauaji haya ya mbunge wa zamani kwenye mtaa wa Bangkok yana dalili zote za mauaji ya kisiasa,” amesema Phil Robertson, mkurugenzi wa shurik lisilo la jiserikali Asia Human Rights Labor Advocates. “Serikali ya Ufaransa itaitajihidi kupata haki kwa raia wake na kuweka shinikizo kwa serikali ya Thailand kufanya uchunguzi wa kina na kuhusu mauaji haya,” ameongeza.

Sam Rainsy anashutumu mauaji ya kisiasa

Mwanasiasa wa upinzani nchini Cambodia Sam Rainsy, aliye uhamishoni nchini Ufaransa, ameshutumu mauaji ya “kisiasa” ya “mwenzake” na “wafanyakazi wa Hun Sen”, ambaye familia yake inaogoza nchi hiyo ya kifalme kwa mkono wa chuma. “Tunaweza kuona mkono wa Hun Sen nyuma ya mauaji ya Lim Kimya kama tulivyoona nyuma ya uhalifu mwingi wa kisiasa nchini Kambodia ambao umesalia bila kuadhibiwa,” aliandika, katika ujumbe kwenye Facebook uliochapishwa usiku wa Jumanne kuamkia Jumatano.

“Kama mimi, Lim Kimya, kama wanaharakati wote wa upinzani wa kidemokrasia, alikuwa kwenye orodha nyeusi ya Hun Sen ambaye haoni aibu kutoka kwa uhalifu wowote. Wanachama kadhaa wa upinzani waliuawa,” amebainisha mpinzani huyo.Lim Kimya ana uraia wa Ufaransa. Aliishi kwa “miaka mingi” huko Ufaransa, anakumbusha Sam Rainsy.

Lim Kimya na Sam Rainsy walichaguliwa kuwa wabunge mwaka wa 2013 chini ya bendera ya Chama cha CNRP, ambacho mafanikio yake ya kihistoria yametishia utawala wa Waziri Mkuu wa wakati huo Hun Sen. Kundi pekee kuu la upinzani lililoanzishwa mwaka wa 2012 na Sam Rainsy na Kem Sokha, CNRP lilivunjwa mwaka wa 2017 na Mahakama ya Juu, na viongozi wake kufunguliwa mashtaka. Wabunge, ikiwa ni pamoja na Lim Kimya, na wanachama wengine wa upinzani walipigwa marufuku kufanya shughuli yotote ya kisiasa. Wengi wamefungwa.

Wakati wa miongo minne akiwa mkuu wa nchi, Hun Sen alishutumiwa mara kwa mara kwa kutumia mahakama kuwafunga mdomo wapinzani wake. Alijiuzulu mnamo 2023 kwa niaba ya mtoto wake, Hun Manet. Mashirika ya haki za binadamu mara nyingi yameshutumu mbinu zake za ukandamizaji kwa mtu yeyote anayekemia makosa, ambayo inaiweka Cambodia miongoni mwa nchi zinazofanya vibaya zaidi barani Asia linapokuja suala la uhuru wa kujieleza au kujumuika.

Msemaji wa serikali ya Cambodia, Pen Bona, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba suala hilo lilikuwa jukumu la mamlaka ya Thailand. Upinzani “daima unashutumu serikali kwa kila kitu, bila msingi au uthibitisho,” alisisitiza, akikataa kuhusika kwa Phnom Penh.

Katika miaka ya hivi karibuni, wanaharakati wa Cambodia wamekimbilia Thailand, lakini wengine wamekamatwa na kuhamishwa hadi nchi yao. Thailand ilikosolewa hapo awali kwa kuwarudisha wakimbizi na wanaotafuta hifadhi katika nchi ambazo usalama wao haukuwa na uhakika.

Ingawa alikuwa na pasipoti ya Ufaransa, Lim Kimya hakutaka kwenda uhamishoni, tofauti na wabunge kadhaa kutoka kambi yake. Wakati wa kuvunjwa kwa chama chake, Lim Kimya alilihakikishia shirika la habari la AFP kwamba “hataacha kamwe siasa”. Ameendelea kutoa maoni yake kwenye Facebook, na katika chapisho lake la mwisho, siku ya Ijumaa, alikashifu kushindwa kwa hafla ya Mwaka Mpya iliyoandaliwa na mwanawe mwingine wa Hun Sen, Hun Many, ambaye kwa sasa ni naibu waziri mkuu.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment