Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Iran inataja matamshi ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron yakitaja nchi hiyo kama “changamoto kuu ya kimkakati na kiusalama” katika Mashariki ya Kati “yhayana msingi”.

Maoni ya Emmanuel Macron “hayana msingi, yanatofautiana na yana lengo la kuchafua”, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei ametangaza siku ya Jumatano Januari 8, akitoa wito kwa Ufaransa “kutafakari upya mbinu zake zisizo za kujenga kwa ajili ya amani na utulivu” katika kanda hiyo, na pia ametaja matamshi ya Emmanuel Macron kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran kuwa “ya kukatisha tamaa”.
Mpango huu ni “wa amani na unaangukia ndani ya mfumo wa sheria za kimataifa,” amesema Esmaeil Baqaei.
Mazungumzo na Marekani juu ya suala la mpango wa nyuklia wa Iran hivi karibuni “yatashughulikiwa tena”
“Iran ndio changamoto kuu ya kimkakati na kiusalama kwa Ufaransa, Wazungu, eneo zima na kwingineko,” Emmanuel Macron alitangaza siku ya Jumatatu Januari 6 mbele ya mabalozi wa Ufaransa waliokusanyika Élysée. “Kuharakishwa kwa mpango wake wa nyuklia kunatuleta karibu sana na hatua ya mdororo,” aliongeza, akibaini kwamba Iran itakuwa suala la kipaumbele katika mazungumzo ambayo atafanya na Rais Mteule wa Marekani Donald Trump.
Emmanuel Macron pia alishutumu kuhusika kwa Tehran “katika vita vya Urusi dhidi ya Ukraine“, “uungaji mkono wake kwa makundi hatari kwenye maeneo yote ya makabiliano katika Mashariki ya Kati” au hata “majaribio yake ya kutumwa barani Afrika. “Katika muktadha huu, swali la Iran bila shaka ni mojawapo ya maswali makuu ambayo tutashiriki tena katika mazungumzo na utawala mpya wa Marekani,” alihitimisha.
Iran imekuwa ikikana kuwa na nia yoyote ya kutengeneza silaha za atomiki. Lakini ni taifa pekee lisilo la nyuklia kumiliki uranium iliyorutubishwa hadi 60%, kulingana na shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA). Kiwango hiki cha uboreshaji ni karibu na 90% muhimu kutengeneza bomu la atomiki.
Mvutano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran uliongezeka wakati wa muhula wa kwanza wa Donald Trump katika Ikulu ya White House, wakati Marekani ilijiondoa katika mkataba wa kihistoria wa mwaka 2015 ambao ulitoa msamaha wa vikwazo vya Tehran badala ya kupunguzwa kwa malengo yake ya nyuklia.
Iran ilishikilia makubaliano hayo hadi Washington ilipojiondoa mnamo mwaka 2018, kisha ikaanza kurejelea kwenye ahadi zake. Inatarajiwa kufanya mazungumzo ya nyuklia na Ufaransa, Uingereza na Ujerumani mnamo Januari 13 nchini Uswisi, chini ya miezi miwili baada ya mazungumzo ya siri na wawakilishi wa nchi hizi tatu huko Geneva.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.