Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mwanamume mmoja alipatikana amefariki Jumatatu asubuhi nje ya kituo cha basi katika eneo la Houston, Texas “kutokana na hali ya hewa ya baridi”, msemaji wa mfumo wa metro wa jiji hilo alithibitisha.
“Mwili ulipatikana kwenye eneo la kuegesha mabasi,” Lester Gretsch, mkurugenzi wa habari wa Mamlaka ya Usafiri wa jiji katika kaunti ya Harris, alisema.
Kifo hicho kinaongeza hadi tano idadi ya vifo vinavyoaminika kusababishwa na Dhoruba ya Majira ya Baridi , ambayo imesababisha theluji na baridi kali katika sehemu kubwa ya Marekani.
Wakati huo huo polisi wanaoshika doria katika barabara kuu ya Jimbo la Missouri waliitikia mwito wa zaidi ya ajali 350 za barabarani.
Watu wawili wamekufa katika ajali mjini Kansas kutokana na hali mbaya ya hewa, mwingine huko Virginia.
Polisi wanasema mwanamume mwenye umri wa miaka 32 alifariki usiku wa manane huko Wakefield, Virginia, baada ya lori lake kuteleza kutoka barabarani na kugonga mti.
Maafisa wanasema alikuwa akiendesha gari kwa kasi sana kwa hali ya barabarani na hakuwa amefunga mkanda, na huenda alikuwa mlevi.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.