Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Utawala wa kijeshi wa Burma umetangaza siku ya Jumamosi, Januari 4, msamaha wa maelfu ya wafungwa, hatua ya kila mwaka kwa mnasaba wa maadhimisho ya uhuru wa nchi hiyo.

Zaidi ya wafungwa 5,800, ikiwa ni pamoja na baadhi ya wageni 180, hivi karibuni watanufaika na hatua hii, utawala wa kijeshi umebainisha katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyonukuliwa na shirika la habari la AFP, wakati Burma inaadhimisha kumbukumbu ya miaka 77 ya uhuru wake, Januari 4, 1948, kutoka kwa Uingereza.
Hakuna habari iliyofichuliwa kuhusu sababu za kufungwa kwao au uraia wa raia wa kigeni wanaohusika ambao watafukuzwa baada ya kuachiliwa, shirika la habari la Ufaransa linabainisha zaidi.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.