Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Apple imekubali kulipa dola milioni 95 ili kutatua kesi inayodai kuwa baadhi ya vifaa vyake vilikuwa vikisikiliza na kurekodi watumiaji bila ruhusa.
Kampuni hiyo kubwa ya teknolojia imeshutumiwa kusikiliza mazungumzo ya wateja wake kupitia programu yake ya usaidizi ya Siri.
Walalamikaji pia wanadai kuwa rekodi za sauti zilishirikiwa kwa watangazaji wa bidhaa.
Apple, inakanusha kufanya makosa yoyote.
Katika juhudi za awali za kutatua tatizo hilo, kampuni hiyo ilikanusha makosa yoyote ya “kurekodi, kufichua taarifa za watu, au kushindwa kufuta mazungumzo yaliyorekodiwa ” bila idhini ya watumiaji.
Mawakili wa Apple pia wanaahidi kuthibitisha kuwa “wamefuta rekodi za sauti za Siri zilizokusanywa na Apple kabla ya mwezi Oktoba, 2019.”
Lakini mashtaka hayo yanasema kampuni hiyo iliwarekodi watu ambao bila kukusudia walianzisha msaidizi wa kawaida bila kutumia neno la siri la “Hey, Siri” linalohitajika kutumia programu.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.