Korea Kusini: Wachunguzi washindwa kumkamata rais aliyeondolewa madarakani

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mwezi mmoja baada ya jaribio lake lililoshindwa la kuweka sheria ya kijeshi, wachunguzi wamejaribu kumkamata rais katika makazi yake rasmi katika mtaa wa Hannam huko Seoul, bila maafanikio. Yoon Suk-yeol anashutumiwa kwa “uasi” na “matumizi mabaya ya mamlaka”. Alitakiwa kuhojiwa, lakini hakutokea alipoitwa na wachunguzi. Wachunguzi wamekambiliwa na upinzani mkali kutoka kwa kitengo cha kijeshi na walinzi wa rais kwa zaidi ya saa nne.

Magari ya wachunguzi kutoka Ofisi ya Maafisa Waandamizi wa Uchunguzi wa Rushwa yakiwasili katika makazi rasmi ya rais wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol, anayekabiliwa na hatua ya kukamatwa kufuatia hati iliyoidhinishwa na mahakama, mjini Seoul, Korea Kusini, Januari 3, 2025.
Magari ya wachunguzi kutoka Ofisi ya Maafisa Waandamizi wa Uchunguzi wa Rushwa yakiwasili katika makazi rasmi ya rais wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol, anayekabiliwa na hatua ya kukamatwa kufuatia hati iliyoidhinishwa na mahakama, mjini Seoul, Korea Kusini, Januari 3, 2025. © Agence de presse Yonhap / via Reuters

Taarifa hiyo ilikuwa ya sehemu na ni vigumu sana kujua ni nini hasa kilikuwa kikiendelea katika makazi ya rais Yoon Suk-yeol, ambapo waandishi wa habari hawakuweza kuyafikia. Tunachojua, kulingana na shirika la habari la Korea Kusini Yonhap, ni kwamba kulikuwa na karibu watu 150 waliotumwa kujaribu kumkamata rais. Maafisa wa polisi na wachunguzi kutoka Ofisi ya Uchunguzi wa Ufisadi wa viongozi wa ngazi za juu serikalini, anaripoti mwandishi wetu huko Seoul, Camille Ruiz.

Walifika mwendo wa saa 1:20 asubuhi kwa saa za ndani, wakiwa wamevalia nguo nyeusi kabisa. Baada ya kupita langoni, wamekabiliwa kwanza na upinzani wa askari, kwa mujibu wa shirika la habari la Yonhap. Lakini maswali bado hayajajibiwa kuhusu uwepo wa wanajeshi hao. Inaonekana ni kikosi cha walinzi wa rais ndiyo waliozuia hali hiyo. Yoon Suk-yeol amesimamishwa kazi, lakini anaendelea na ulinzi huu, kwa sababu bado yuko ana mamlaka ya rais. Mmoja wa mawakili wake aliwasili katika eneo la tukio majira ya saa 6:30.

Ofisi Kuu ya Upelelezi wa Ufisadi (CIO), ambayo inaweka uchunguzi kati, ina hadi Januari 6 kutekeleza hati ya kukamatwa iliyotolewa na mahakama kwa ombi lake ambalo halijawahi kushuhudiwa dhidi ya mkuu wa nchi wa Korea Kusini. Rais aliyeondolewa madarakani, ambaye haruhusiwi kuondoka nchini humo, alikuwa katika makazi yake rasmi mjini Seoul, wakili wake amelithibitishia shirika la habari la AFP. Timu yake ya wanasheria imewasilisha rufaa dhidi ya hati ya kukamatwa, ikisema kuwa “ni kinyume cha sheria na ni batili.”

CIO iliomba hati ya kukamatwa baada ya rais aliyeondolewa madarakani, ambaye anachunguzwa kwa “uasi” – uhalifu unaoadhibiwa kifo – kupuuza wito wa tatu mfululizo wa kuhojiwa.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment