Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mateka mmoja anayeshikiliwa na kundi la wanamgambo wa Islamic Jihad huko Gaza amejaribu kujiua, msemaji wa kundi hilo amesema katika video iliyowekwa kwenye Telegram siku ya Alhamisi.
“Timu ya madaktari wa kundi hilo iliingilia kati na kumzuia asife,” aliongeza msemaji wa Brigedi ya Al Quds, bila ya kufafanua zaidi juu ya utambulisho wa mateka au hali yake ya sasa.
Israel bado haijatoa kauli yoyote.
Zaidi ya mwaka mmoja baada ya mashambulizi yanayoongozwa na Hamas dhidi ya Israel, jumla ya mateka 96 hawajulikani waliko.
Kulingana na Israel, Waisraeli 251 na wageni walitekwa Oktoba 7, 2023. Idadi rasmi ya Waisraeli walioshikiliwa huko Gaza ni 101 – ikijumuisha watu wanne waliotekwa nyara 2014 na 2015. Wawili kati yao wanaaminika kufariki.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.