Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Zaidi ya watu 70 wamefariki katika ajali ya barabarani kusini mwa Ethiopia siku ya Jumapili Desemba 29, polisi imetangaza katika ripoti mpya, ikibainisha kuwa gari lililokuwa likiwasafirisha wahanga lilianguka kwenye korongo.

Gari la Isuzu, aina ya gari lililotengenezwa Japani linalojulikana kwa magari yake ya matumizi, “lilianguka kwenye bonde la Mto Gelana,” polisi imesema katika taarifa Jumapili jioni, kimnukuu kamishna wa polisi wa mkoa Daniel Sankura.
Ofisi ya Afya ya Jimbo la Sidama imesema kwenye Facebook siku ya Jumapili jioni kwamba “ajali ya barabarani imegharimu maisha ya watu 66 hadi sasa,” bila kutoa maelezo zaidi. Jimbo la Sidama liko takriban kilomita 300 kusini mwa mji mkuu Addis Ababa.
Ameongeza kuwa watu wanne walikuwa wakitibiwa katika Hospitali Kuu ya Bona. Picha zenye ukungu zilizotolewa na Ofisi ya Afya zinaonyesha watu wengi wakizunguka gari, wakiwa wamezama kwa kiasi kwenye maji.
Daniel Sankura amesema wanaume 68 na wanawake watatu walipoteza maisha katika ajali hiyo, na watu wengine wawili walijeruhiwa vibaya.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.