Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Wahadhiri na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Marien Ngouabi mjini Brazzaville wanarejea shuleni leo Jumatatu, Desemba 30. Kufuatia maendeleo ya mazungumzo yaliyoanzishwa na serikali, walimu wameamua kusitishwa mgomo wao uliyoanza Oktoba 1.

Kulingana na Jean Didier Mbélé, rais wa muungano wa vyama vya wafanyakazi, serikali imejitolea kulipa mishahara ya miezi miwili, kati ya minne inayodaiwa, na sasa kulipa mishahara ya walimu mara kwa mara.
“Vyama vya wafanyakazi katika Chuo Kikuu cha Marien Ngouabi vilijadiliana na serikali na uongozi wa Chuo Kikuu cha Marien Ngouabi. Tulitia saini taarifa ya hitimisho ambapo serikali ilitulipa mishahara ya miezi miwili, kati ya miezi minne tuliyopaswa kulipwa: Novemba na Desemba 2024, pamoja na saa zingine za muda wa ziada zinazopaswa kulipwa mwaka wa 2021 na 2022,” amesema Jean Didier Mbelé.
Akiwa na furaha tele kuanza tena masomo tarehe 30 Desemba na kuamini katika ahadi mbalimbali za serikali, Bw. Jean Didier Mbélé amesema: “serikali pia imejitolea kutulipa mara kwa mara kuanzia sasa”.
Visomo vilivyorekebishwa
Ameongeza: “Hatukuweza kuruhusu mwaka wende kombo kwa sababu mfumo wa LMD (Leseni – Shahada ya Uzamili) hauruhusu. Tuna wasiwasi kuhusu vijana ambao ni mustakabali wa nchi.”
Jean Didier Mbélé ameahidi: “hatutaweza kamwe kuacha kusoma baadhi ya visomo. Mkuu wa chuo kikuu Mrien Ngouabi atapanga upya kalenda ya visomo, kulingana na viwango vya UNESCO ambavyo hutoa na kuhitaji wiki 25 za kusoma kwa mwaka mzima wa masomo.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.