Ecuador: Utata waongezeka baada ya vifo vya vijana wanne waliochomwa moto

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mnamo Desemba 8, watoto wanne walitoweka huko Guayaquil, kusini-magharibi mwa Ecuador, baada ya mechi ya kandanda. Hapo awali waliwasilishwa kama wahalifu, wavulana – Josué Arroyo (umri wa miaka 15), Ismael Arroyo (umri wa miaka 14), Saul Arboleda (umri wa miaka 11) na Steven Medina (umri wa miaka 15) –  ni waathiriwa wa kosa la kijeshi.

Mwanamke huyu ameshikilia bango wakati wa maandamano huko Quito, Desemba 23, 2024, dhidi ya kutoweka kwa vijana wanne wakati wa operesheni ya kijeshi.
Mwanamke huyu ameshikilia bango wakati wa maandamano huko Quito, Desemba 23, 2024, dhidi ya kutoweka kwa vijana wanne wakati wa operesheni ya kijeshi. © GALO PAGUAY – AFP

Siku chache baada ya kutoweka, polisi waligundua miili minne iliyoungua kabisa katika eneo la kipekee la mikoko. Watoto hao walipelekwa eneo hili karibu na kambi ya jeshi la anga la Taura na askari wa doria wa jeshi la anga la Ecuador. Polisi walilazimika kuvuka maji yenye matope ili kuchimba mabaki ya binadamu, anaripoti mwandishi wetu huko Quito, Éric Samson.

Kwa mujibu wa mamlaka, kutokana na kukosekana kwa alama za vidole zinazoweza kutumika, madaktari wa kuchunguza maiti watalazimika kuchunguza maiti ili kubaini makovu au alama za upasuaji unaoruhusu utambuzi wao. Ikiwa hii itashindwa, vipimo vya DNA, matokeo ambayo itachukua wiki kadhaa, vitakuwa muhimu.

Waziri wa Ulinzi anabaini kwamba “vijana waliachiliwa usiku”

Picha za kamera za uchunguzi zilionyesha wavulana wawili wakilazimishwa kuingia kwenye gari la kijeshi na kufanyiwa dhulma. Katika video iliyorushwa na Bunge la taifa, kijana mwingine anaonekana kifudifudi ndani ya gari la kijeshi.

Waziri wa Ulinzi Gian Carlo Loffredo awali alidai kuwa watoto hao walikuwa wametekwa nyara na kundi la wahalifu. Kutokana na ugunduzi huo, amebadilisha hotuba yake, na kutangaza kwamba “vijana walikuwa wameachiliwa usiku” na kwamba walikamatwa na wahalifu. Ufafanuzi unaopingwa sana na familia na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Raia wapandwa na hasira

Jambo hili limesababisha hasira kubwa huko Ecuador. Huko Guayaquil na Quito, mamia ya watu wameandamana kudai haki na ukweli. “Tafadhali muturudishie wakiwa hai,” amesihi Luis Arroyo, baba wa ndugu wawili waliotoweka.

Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu (IACHR) imeonyesha “wasiwasi wake mkubwa”, wakati Umoja wa Mataifa na UNICEF wametaka ufanyike uchunguzi “wa kina, wa haraka na usio na upendeleo”.

Ofisi ya mwendesha mashtaka wa Ecuador imevamia kambi ya jeshi la anga ya Taura, na kukamata simu na magari ya wanajeshi.

Kesi inayotikisa taasisi

Tukio hili la kuhuzunisha limeleta pigo kubwa kwa picha ya jeshi la Ecuador, nguzo kuu ya sera ya usalama ya Rais Daniel Noboa. Chini ya shinikizo, aliamuru kwenye mtandao wa kijamii wa X, “kuimarishwa kwa hatua zote muhimu za kuwatafuta watoto hao wanne na kuwatafuta wote waliohusika ili waweze kujibu kwa matendo yao mbele ya mahakama na nchi”.

Kwa muda mrefu ikizingatiwa kama kimbilio la amani kati ya Colombia na Peru, nchi kuu zinazouza kokeini, Ecuador imeshuhudia vurugu zikilipuka katika miaka ya hivi karibuni. Magenge hasimu yanayohusishwa na magenge ya Mexico na Colombia yanapigania kudhibiti ulanguzi nchini humo, ambao umekuwa ungo mkubwa wa uzalishaji wa dawa za kulevya.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment