AFRIKA LEO JIONI-23-12-2024

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Karibu katika Matangazo yetu ya jioni moja kwa moja kutoka Communication Center. Tumekuandalia mengi ikiwa ni pamoja

Muhtasari

  • Maafisa wa zamani wa Israeli wafichua vile vifaa vya mawasiliano yalitekelezwa
  • Msumbiji ina wasiwasi huku ikisubiri uamuzi kuhusu uchaguzi wenye utata
  • Ujumbe wa Urusi umewasili Iran kukutana na rais
  • Ahmed Al-Sharaa: Makundi yenye silaha nchini Syria yatasambaratishwa na kuunganishwa katika jeshi
  • Rais mteule Trump na mwenzake wa Panama warushiana cheche za maneno
  • Korea Kaskazini inajiandaa kutuma wanajeshi zaidi Urusi
  • Waziri Mkuu wa Slovakia akutana na Putin katika ziara ya kushtukiza mjini Moscow
  • Papa Francis atoa wito wa kusitishwa kwa mapigano katika maeneo yote wakati wa Krisimasi
  • Mwanamke afariki baada ya kuchomwa moto kwenye treni ya chini ya ardhi New York
  • Urusi na Ukraine: ‘Putin anataka kuniona haraka iwezekanavyo’ – Trump

Naam,Natumai U buheri wa afya popote pale ulipo duniani kwa mwoyo mkunjufu na mikono miwili Hujambo na karibu katika matangazo yetu Afrika Leo Jioni ya moja kwa moja ikiwa ni tarehe 23/12/2024 Jina langu ni Cantona Joseph,karibu.

Joe Biden amepunguza adhabu ya kifo kwa wafungwa 37

.

Rais Joe Biden amepunguza adhabu za kifo za wafungwa 37 kati ya 40 waliokuwa na hukumu ya kifo, na kubadilisha adhabu zao kuwa kifungo cha maisha bila kifungo cha nje.

Hata hivyo, wafungwa watatu, wakiwemo washukiwa wa bomu la Boston na muuaji wa waabudu wa Kiyahudi mwaka 2018, hawakupunguziwa adhabu.

Biden alisema anaamini kuwa adhabu ya kifo inapaswa kuondolewa. Hatua hii haijahusisha zaidi ya wafungwa 2,000 waliokata rufaa kwenye mahakama za majimbo.

Zaidi ya visa 70 za wafungwa kunyongwa katika majimbo vimetekelezwa wakati wa utawala wa rais Joe Biden.

Biden ameonyesha kupinga adhabu ya kifo na alisimamisha utekelezaji wake wakati alipoingia madarakani.

Hata hivyo, rais wa Marekani ajaye Donald Trump alirudisha utekelezaji wa adhabu ya kifo wakati alipoongoza muhula wa kwanza.

Biden pia ameendelea kutoa msamaha kwa wafungwa wengine, ikiwa ni pamoja na kumsamehe mwanawe Hunter Biden kwa mashtaka ya uhalifu.

Hunter alikuwa amekiri makosa yake mwezi Septemba na kupatikana na hatia ya kuwa mtumizi wa dawa za kulevya mwezi Juni na kuwa mtoto wa kwanza wa rais kushtakiwa kwa makosa ya uhalifu.

Katiba ya Marekani inaamuru kwamba rais ana “mamlaka mapana ya kutoa msamaha, isipokuwa katika kesi zinazohusiana na kuenguliwa”.

Maafisa wa zamani wa Israeli wafichua jinsi mashambulizi ya vifaa vya mawasiliano yalitekelezwa

.

Maafisa wawili wa zamani wa kijasusi wa Israel wamefichua jinsi wanachama wa kundi la wanamgambo wa Shia wa Lebanon Hezbollah walivyotumia Israel kutengeneza vifaa vya mawasiliano vilivyonaswa na vilipuzi kwa miaka 10 kabla ya kulipuliwa katika shambulio la kushtukiza Septemba mwaka huu.

Maafisa hao wawili wa zamani wa Mossad waliambia shirika la habari la CBS la Marekani jinsi huduma hiyo ilivyowalaghai Hezbollah katika kununua maelfu ya vifaa vya mawasiliano bila kutambua kuwa vilitengenezwa Israeli.

Makumi ya watu waliuawa na maelfu kujeruhiwa katika mashambulizi hayo. Israeli ilisema vifaa hivyo vilitengenezwa kulenga wanachama wa Hezbollah pekee, lakini raia walikuwa miongoni mwa waathiriwa, maafisa wa Lebanon walisema.

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amelitaja shambulio hilo kuwa uhalifu wa kivita.

Wakati wa shambulio hilo, Israeli na Hezbollah walikuwa wakipigana. Mzozo ambao uliongezeka tangu Hezbollah ilipofyatua risasi kwenye maeneo ya Israeli siku moja baada ya shambulio la Hamas kusini mwa Israeli tarehe 7 Oktoba 2023.

Jinsi yalivyopangwa

Katika mahojiano na mshirika wa utangazaji wa BBC nchini Marekani , maafisa hao wawili wa zamani walifichua maelezo ya operesheni hiyo.

Mmoja wao aliyepewa jina la Michael, alisema Mossad walikuwa wameficha kifaa cha kulipuka ndani ya betri zinazotumia vifaa hivyo, ambavyo alisema kwa kawaida hubebwa kwenye fulana karibu na moyo wa mvaaji.

Alisema Hezbollah ilinunua bila kujua zaidi ya vifaa 16,000 kwa “bei nzuri” kutoka kwa kampuni bandia miaka 10 iliyopita.

“Tuna uweze mkubwa wa kutengeneza kampuni za kigeni ambazo hazina njia ya kufuatiliwa hadi Israeli,” Michael alisema. “Makampuni ya Shell juu ya makampuni ya shell ili kuathiri ugavi kwa manufaa yetu.

“Tunatengeneza dunia ya isiokuwepo. Sisi ni kampuni ya utazalishaji kimataifa. Tunaandika filamu, sisi ni waelekezi, sisi ni watayarishaji, sisi ni waigizaji wakuu, na ulimwengu ni jukwaa letu.”

Msumbiji ina wasiwasi huku ikisubiri uamuzi kuhusu uchaguzi wenye utata

.

Kuna hali ya wasiwasi katika mji mkuu wa Msumbiji, Maputo, wakati nchi hiyo ikisubiri uamuzi wa mahakama kuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais uliopingwa wa Oktoba, ambao ulipotangazwa kwa mara ya kwanza ulizua maandamano mabaya ya wiki kadhaa.

Venâncio Mondlane, ambaye aliibuka wa pili kulingana na hesabu rasmi, amekuwa akitoa wito kwa wafuasi wake kwa muda mrefu wa miezi miwili iliyopita kuandamana dhidi ya kile alichosema kuwa kura iliyoibiwa.

Mondlane, mwenyewe, yuko uhamishoni baada ya kuikimbia nchi akiwashutumu polisi kwa tabia ya vitisho muda mfupi baada ya wasaidizi wake wawili kuuawa kwa kupigwa risasi mwezi Oktoba.

Katika ujumbe wake wa wikendi kwenye mtandao wa kijamii, alisema kunaweza kuwa na “machafuko mapya” ikiwa matokeo hayatabatilishwa.

Ujumbe wa Urusi umewasili Iran kukutana na rais

.

Ujumbe wa Urusi umewasili Tehran kwa ziara inayojumuisha mkutano na Rais wa Iran Masoud Pezeshkian, shirika la habari la Urusi TASS liliripoti Jumatatu, wakati nchi hizo mbili zikijiandaa kutia saini makubaliano ya ushirikiano wa kina.

Iran na Urusi zimekuwa zikifanya kazi ya kupanga tarehe ya kukamilisha makubaliano, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baghaei alisema Jumatatu, na kuongeza kuwa makubaliano hayo yanatazamiwa kutiwa saini katika ziara ya pande mbili mwezi Januari.

Urusi imekuza uhusiano wa karibu na Iran na nchi nyingine zenye uadui dhidi ya Marekani, kama vile Korea Kaskazini, tangu kuanza kwa vita vya Ukraine.

Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Sergei Lavrov alisema mwezi Oktoba kwamba Moscow na Tehran zinakusudia kusaini makubaliano ambayo yatajumuisha ushirikiano wa karibu wa kiulinzi.

Ujumbe wa Urusi nchini Iran unaongozwa na naibu waziri mkuu Alexei Overchuk na Vitaly Savelev, kwa mujibu wa shirika la habari la Interfax la Urusi.

Msumbiji ina wasiwasi huku ikisubiri uamuzi kuhusu uchaguzi wenye utata

.

Kuna hali ya wasiwasi katika mji mkuu wa Msumbiji, Maputo, wakati nchi hiyo ikisubiri uamuzi wa mahakama kuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais uliopingwa wa Oktoba, ambao ulipotangazwa kwa mara ya kwanza ulizua maandamano mabaya ya wiki kadhaa.

Venâncio Mondlane, ambaye aliibuka wa pili kulingana na hesabu rasmi, amekuwa akitoa wito kwa wafuasi wake kwa muda mrefu wa miezi miwili iliyopita kuandamana dhidi ya kile alichosema kuwa kura iliyoibiwa.

Mondlane, mwenyewe, yuko uhamishoni baada ya kuikimbia nchi akiwashutumu polisi kwa tabia ya vitisho muda mfupi baada ya wasaidizi wake wawili kuuawa kwa kupigwa risasi mwezi Oktoba.

Katika ujumbe wake wa wikendi kwenye mtandao wa kijamii, alisema kunaweza kuwa na “machafuko mapya” ikiwa matokeo hayatabatilishwa.

Ujumbe wa Urusi umewasili Iran kukutana na rais

.

Ujumbe wa Urusi umewasili Tehran kwa ziara inayojumuisha mkutano na Rais wa Iran Masoud Pezeshkian, shirika la habari la Urusi TASS liliripoti Jumatatu, wakati nchi hizo mbili zikijiandaa kutia saini makubaliano ya ushirikiano wa kina.

Iran na Urusi zimekuwa zikifanya kazi ya kupanga tarehe ya kukamilisha makubaliano, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baghaei alisema Jumatatu, na kuongeza kuwa makubaliano hayo yanatazamiwa kutiwa saini katika ziara ya pande mbili mwezi Januari.

Urusi imekuza uhusiano wa karibu na Iran na nchi nyingine zenye uadui dhidi ya Marekani, kama vile Korea Kaskazini, tangu kuanza kwa vita vya Ukraine.

Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Sergei Lavrov alisema mwezi Oktoba kwamba Moscow na Tehran zinakusudia kusaini makubaliano ambayo yatajumuisha ushirikiano wa karibu wa kiulinzi.

Ujumbe wa Urusi nchini Iran unaongozwa na naibu waziri mkuu Alexei Overchuk na Vitaly Savelev, kwa mujibu wa shirika la habari la Interfax la Urusi.

Ahmed Al-Sharaa: Makundi yenye silaha nchini Syria yatasambaratishwa na kuunganishwa katika jeshi

.

Kiongozi mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa amesema kuwa silaha zote zitakuwa chini ya udhibiti wa serikali kuu zikiwemo zile zinazoshikiliwa na vikosi vya Wakurdi.

Alisema katika mkutano na waandishi wa habari baada ya kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan mjini Damascus kwamba makundi yenye silaha yatatangaza hivi karibuni kuvunjwa kwao na kujiunga na jeshi jipya la Syria, lakini hakutoa muda kamili kwa hili.

Hakan Fidan pia alisisitiza kwamba Wasyria walikuwa na jukumu la kumpindua Bashar al-Assad, na katika hotuba yake kwa viongozi wa Kamati ya Tahrir al-Sham, alisema: “Ushindi huu ni wako tu, si wa mtu mwingine yeyote. kufaidika na fursa ya kihistoria kwa kujitolea kwako.”

Türkiye ndiye mfuasi mkuu wa kundi la Tahrir al-Sham, lililonyakua mamlaka nchini Syria takriban wiki mbili zilizopita.

Ahmed Al-Sharaa: Makundi yenye silaha nchini Syria yatasambaratishwa na kuunganishwa katika jeshi

.

Kiongozi mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa amesema kuwa silaha zote zitakuwa chini ya udhibiti wa serikali kuu zikiwemo zile zinazoshikiliwa na vikosi vya Wakurdi.

Alisema katika mkutano na waandishi wa habari baada ya kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan mjini Damascus kwamba makundi yenye silaha yatatangaza hivi karibuni kuvunjwa kwao na kujiunga na jeshi jipya la Syria, lakini hakutoa muda kamili kwa hili.

Hakan Fidan pia alisisitiza kwamba Wasyria walikuwa na jukumu la kumpindua Bashar al-Assad, na katika hotuba yake kwa viongozi wa Kamati ya Tahrir al-Sham, alisema: “Ushindi huu ni wako tu, si wa mtu mwingine yeyote. kufaidika na fursa ya kihistoria kwa kujitolea kwako.”

Türkiye ndiye mfuasi mkuu wa kundi la Tahrir al-Sham, lililonyakua mamlaka nchini Syria takriban wiki mbili zilizopita.

Rais mteule Trump na mwenzake wa Panama warushiana cheche za maneno

.

Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa wito wa kupunguzwa kwa ushuru wa forodha kwa kutumia rasi ya Panama la sivyo airejeshe chini ya usimamiz wa Marekani Bw. Trump ameishutumu Panama kwa kuweka “gharama kubwa” kwa usafiri wa majini na Jeshi la Wanamaji la Marekani.

“Viwango hivi ambavyo Panama imeweka ni vya kipuuzi na si vya haki kabisa,” Bw. Trump aliuambia umati wa wafuasi huko Arizona. “Huu wembe utakoma mara moja,” alisema, akimaanisha mwezi atakaoingia madarakani.

Rais wa Panama alijibu mara moja kauli za Bw. Trump, akisema, “Kila inchi ya Mfereji wa Panama na maeneo yanayoizunguka ni ya Panama.”

Rais wa Panama Jose Raul Molino aliongeza kuwa uhuru wa nchi yake ni jambo lisiloweza kujadiliwa.

Korea Kaskazini inajiandaa kutuma wanajeshi zaidi Urusi

.

Korea Kaskazini inaonekana kujiandaa kutuma wanajeshi wa ziada nchini Urusi kushiriki katika vita na Ukraine, pamoja na vifaa vya kijeshi, zikiwemo ndege zisizo na rubani za kamikaze, ripoti ya Yonhap, ikiwanukuu maafisa wa kijeshi wa Korea Kusini.

“Tathmini ya kina ya vyanzo vingi vya kijasusi inaonyesha kuwa Korea Kaskazini inajiandaa kuongeza idadi ya wanajeshi [nchini Urusi],” shirika hilo linanukuu Wakuu wa Pamoja wa wanajeshi wa Korea Kusini wakisema.

Ujasusi wa Korea Kusini hapo awali ulikadiria hasara ya wanajeshi wa DPRK katika vita hivyo kuwa takriban watu 1,100 – idadi hii inajumuisha askari waliouawa (watu 100) na waliojeruhiwa.

“Pia kuna baadhi ya dalili kwamba Kaskazini inaelekea kuzalisha na kusambaza ndege zisizo na rubani za Kamikaze, ambazo zilifichuliwa kwa mara ya kwanza wakati wa ukaguzi wa Kim Jong-un mnamo Novemba,” kamati hiyo iliongeza.

Vyombo vya habari vya Korea Kaskazini viliripoti kwamba Kim Jong-un alisimamia majaribio ya aina mbalimbali za ndege zisizo na rubani mwezi Novemba na kutoa wito wa kuzalishwa kwa wingi, Yonhap imeandika.

Rais mteule Trump na mwenzake wa Panama warushiana cheche za maneno

.

Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa wito wa kupunguzwa kwa ushuru wa forodha kwa kutumia rasi ya Panama la sivyo airejeshe chini ya usimamiz wa Marekani Bw. Trump ameishutumu Panama kwa kuweka “gharama kubwa” kwa usafiri wa majini na Jeshi la Wanamaji la Marekani.

“Viwango hivi ambavyo Panama imeweka ni vya kipuuzi na si vya haki kabisa,” Bw. Trump aliuambia umati wa wafuasi huko Arizona. “Huu wembe utakoma mara moja,” alisema, akimaanisha mwezi atakaoingia madarakani.

Rais wa Panama alijibu mara moja kauli za Bw. Trump, akisema, “Kila inchi ya Mfereji wa Panama na maeneo yanayoizunguka ni ya Panama.”

Rais wa Panama Jose Raul Molino aliongeza kuwa uhuru wa nchi yake ni jambo lisiloweza kujadiliwa.

Waziri Mkuu wa Slovakia akutana na Putin katika ziara ya kushtukiza mjini Moscow

.

Waziri Mkuu wa Slovakia Robert Fico amefanya ziara ya kushtukiza mjini Moscow kwa mazungumzo na Vladimir Putin – akiwa ni kiongozi wa tatu pekee wa nchi za Magharibi kukutana na kiongozi huyo wa Urusi tangu uvamizi kamili wa Ukraine miaka mitatu iliyopita.

Fico – mkosoaji mkubwa wa uungaji mkono wa Umoja wa Ulaya kwa Kyiv katika vita – alisema walijadili usambazaji wa gesi ya Urusi kwa Slovakia – ambayo nchi yake inaitegemea.

Mkataba na kampuni kubwa ya gesi ya Gazprom ya kusafirisha nishati kupitia Ukraine hadi Slovakia unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwaka huu.

“Maafisa wakuu wa EU walifahamishwa kuhusu safari yangu na madhumuni yake… siku ya Ijumaa,” Fico aliandika kwenye Facebook.

Korea Kaskazini inajiandaa kutuma wanajeshi zaidi Urusi

.

Korea Kaskazini inaonekana kujiandaa kutuma wanajeshi wa ziada nchini Urusi kushiriki katika vita na Ukraine, pamoja na vifaa vya kijeshi, zikiwemo ndege zisizo na rubani za kamikaze, ripoti ya Yonhap, ikiwanukuu maafisa wa kijeshi wa Korea Kusini.

“Tathmini ya kina ya vyanzo vingi vya kijasusi inaonyesha kuwa Korea Kaskazini inajiandaa kuongeza idadi ya wanajeshi [nchini Urusi],” shirika hilo linanukuu Wakuu wa Pamoja wa wanajeshi wa Korea Kusini wakisema.

Ujasusi wa Korea Kusini hapo awali ulikadiria hasara ya wanajeshi wa DPRK katika vita hivyo kuwa takriban watu 1,100 – idadi hii inajumuisha askari waliouawa (watu 100) na waliojeruhiwa.

“Pia kuna baadhi ya dalili kwamba Kaskazini inaelekea kuzalisha na kusambaza ndege zisizo na rubani za Kamikaze, ambazo zilifichuliwa kwa mara ya kwanza wakati wa ukaguzi wa Kim Jong-un mnamo Novemba,” kamati hiyo iliongeza.

Vyombo vya habari vya Korea Kaskazini viliripoti kwamba Kim Jong-un alisimamia majaribio ya aina mbalimbali za ndege zisizo na rubani mwezi Novemba na kutoa wito wa kuzalishwa kwa wingi, Yonhap imeandika.

Waziri Mkuu wa Slovakia akutana na Putin katika ziara ya kushtukiza mjini Moscow

.

Waziri Mkuu wa Slovakia Robert Fico amefanya ziara ya kushtukiza mjini Moscow kwa mazungumzo na Vladimir Putin – akiwa ni kiongozi wa tatu pekee wa nchi za Magharibi kukutana na kiongozi huyo wa Urusi tangu uvamizi kamili wa Ukraine miaka mitatu iliyopita.

Fico – mkosoaji mkubwa wa uungaji mkono wa Umoja wa Ulaya kwa Kyiv katika vita – alisema walijadili usambazaji wa gesi ya Urusi kwa Slovakia – ambayo nchi yake inaitegemea.

Mkataba na kampuni kubwa ya gesi ya Gazprom ya kusafirisha nishati kupitia Ukraine hadi Slovakia unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwaka huu.

“Maafisa wakuu wa EU walifahamishwa kuhusu safari yangu na madhumuni yake… siku ya Ijumaa,” Fico aliandika kwenye Facebook.

Papa Francis atoa wito wa kusitishwa kwa mapigano katika maeneo yote wakati wa Krisimasi

.

Papa alishutumu mashambulizi ya kikatili ya shule na hospitali nchini Ukraine na Gaza katika sala yake ya Jumapili kabla ya Krismasi.

“Wacha bunduki zinyamaze na nyimbo za Krismasi zisikie!” Francis alisema wakati wa maombi yake siku ya Jumapili, ambayo aliitoa ndani ya kanisa hilo kama tahadhari kabla ya kipindi cha Krismasi chenye shughuli nyingi.

“Hebu tuombe kwamba Siku ya Krismasi kuwe na usitishaji wa mapigano katika nyanja zote za vita, nchini Ukraine, katika ardhi takatifu, Mashariki ya Kati na ulimwenguni kote,” papa alisema.

Francis alikumbuka, kama anavyofanya mara nyingi, mateso ya wanayopitia raia wa Ukraine, ambayo miji yake inaendelea kushambuliwa, “wakati fulani huharibu shule, hospitali na makanisa.”

Pia alisema alihisi uchungu alipofikiria kuhusu Gaza, “ukatili kama huo, bunduki zinazoua watoto, kulipua shule na hospitali.”

Mwanamke afariki baada ya kuchomwa moto kwenye treni ya chini ya ardhi New York

.

Mwanamume mmoja amekamatwa huko New York kuhusiana na kifo cha mwanamke aliyechomwa moto kwenye treni ya chini ya ardhi huko Brooklyn.

Kamishna wa polisi Jessica Tisch alielezea tukio hilo la Jumapili kama “moja ya uhalifu mbaya ambao mtu anaweza kufanya dhidi ya binadamu mwingine”.

Alisema mwanamke huyo alikuwa kwenye treni ya F kuelekea Brooklyn alipofikiwa na mwanamume aliyetumia kiberiti kuwasha mavazi yake.

Mwathiriwa alifariki katika eneo la tukio, alisema, na kuongeza kuwa mshukiwa alikamatwa kufuatia taarifa kutoka kwa kundi la wanafunzi wa shule ya upili alipoonekana ktika kituo hicho cha treni ardhi baadaye Jumapili.

Polisi wanasema mwanamke huyo, ambaye hajatajwa jina, alikuwa kwenye treni ya chini ya ardhi katika kituo cha Coney Island-Stillwell Avenue huko Brooklyn yapata saa 07:30 saa za huko (12:30 GMT) wakati mwanamume huyo alipomfuata.

Hakukuwa na mwingiliano kabla ya shambulio hilo, polisi walisema, na kuongeza kuwa hawakuamini kuwa watu hao wawili walifahamiana.

Mwanamume huyo alishuka kwenye treni huku maafisa wa polisi waliokuwa wakishika doria katika kituo hicho wakikimbilia eneo la tukio.

“Maafisa walikuwa wakishika doria katika ngazi ya juu ya kituo hicho, wakanusa na kuona moshi na kwenda kuchunguza,” Bi Tisch alisema.

“Walichoona ni mtu aliyesimama ndani ya gari la moshi akiwa amezingirwa na moto.”

Polisi bado wanachunguza chanzo cha tukio hilo

Urusi na Ukraine: ‘Putin anataka kuniona haraka iwezekanavyo’ – Trump

.
Maelezo ya picha,Putin na Trump

“Rais Putin anasema anataka kukutana nami haraka iwezekanavyo,” Trump alisema katika kongamano huko Arizona. “Kwa hivyo itabidi tusubiri, lakini lazima tukomeshe vita hivi. Vita hivi vinatisha, vinatisha.”

Trump, ambaye atarejea Ikulu ya White House mwezi Januari, awali alisema wakati wa kampeni kwamba akichaguliwa kuwa rais anaweza kumaliza vita hivyo chini ya saa 24.”

Hivi majuzi alikosoa uidhinishaji wa Biden kwa Ukraine kutumia silaha za masafa marefu zilizotolewa na Marekani kushambulia eneo la Urusi.

“Idadi ya wanajeshi waliouawa… Ni ardhi tambarare, na risasi zinapaa, risasi zenye nguvu, bunduki zenye nguvu, na kitu pekee kinachoweza kuzuia ni mwili wa binadamu,” Trump alisema, akisisitiza kwamba vita vya Ukraine visingefanyika iwapo angekuwa rais wa Marekani wakati huo.

Kampuni ya sukari ya Sony Sugar nchini Kenya yarejelea shughuli baada ya kurekebisha mitambo

Trekta ikisafirisha miwa kwenye barabara kuu ya Kisii – Migori awali 2018. PICHA | MAKTABA

KIWANDA cha kutengeneza sukari cha Sony katika Kaunti ya Migori  wikendi kilirejelea shughuli zake baada ya kufungwa kwa wiki mbili ili kurekebisha mitambo yake.

Urekebishaji huo uligharimu Sh300 milioni na ulilenga kuhakikisha kuwa kiwanda hicho kinaendesha operesheni zake kikamilifu bila mitambo kuharibika kila mara.

Hitilafu hizo za kimitambo zimekuwa na athari kubwa za kifedha kwa kiwanda hicho cha sukari.

“Mitambo hiyo ilikuwa katika hali mbaya na kufanya iwe vigumu kwa kiwanda kutimiza malengo yake, jambo ambalo limetusababishia hasara tele,” akasema Meneja Mkurugenzi Martine Dima.

Wahudumu shambani wakipakia miwa kwa trekta mnamo Aprili 2024 kupeleka kiwandani. PICHA | ISAAC WALE

Bw Dima alisema kuwa wanatarajia marekebisho hayo yatapiga jeki shuguhuli ziendelee kwa angalau miezi sita mfululizo bila tatizo lolote.

Alifichua kwamba kiwanda hicho kitafungwa tena Mei 2025 ili kufanyiwa ukarabati wa kina ikiwemo kuondoa kabisa mitambo ya zamani na kuweksa mipya.

Afisa mkuu huyo alieleza kwamba mitambo ya zamani haikuwa imerekebishwa au kubadilishwa kwa miezi 12 ndiposa kiwanda hicho hakikuwa kinatimiza viwango vya uzalishaji.

Baada tu ya kuteuliwa kama mkurugenzi wa Sony mnamo Mei 2024, Bw Dima aliweka kipaumbele mipango ya kutunza rasilimali na kuongeza kiwango cha uzalishaji ili kukatiza mtindo wa kutegemea ufadhili wa serikali kwa kila jambo katika operesheni zzao.

Kiwanda hicho kilianzishwa mnamo 1978 na kinastahili kusaga tani 3,000 za miwa kila siku. Hata hivyo, kimeandamwa na changamoto tele ikiwemo hitilafu za mitambo, ambao umedidimiza usagaji miwa.

Huku akikiri kuwa changamoto zinazonga kiwanda hicho bado ni nyingi, Bw Dima alikuwa na imani kwamba ukarabati wa kina ambao wamepanga kutekeleza mwakani utaimarisha sio tu mapato ya kampuni bali pia ya wakuzaji miwa.

“Shughuli hizi za ukarabati zinalenga kuhakikisha operesheni za kiwanda zinaendelea bila tatizo na kurejesha matumaini kwa wakulima na washikadau wa miwa katika ukanda huu kwamba kilimo cha miwa kina natija,” akasema.

Mkulima akivuna miwa shambani awali 2016. PICHA | MAKTABA

Meneja huyo mkurugenzi alihimiza wakulima wa hapo kuongeza kiwango cha ekari wanakokuza miwa ili kiwanda kiwategemee badala ya kununua zao hilo kutoka maeneo mengine na hivyo kutatizikia gharama ya usafiri.

Kampuni ya Sony ina ekari 2,400 za ardhi ambako kinakuza miwa japo pia wakulima wa kibinafsi wanakuza miwa katika ekari nyingine 6,000 na kuwasilisha katika kiwanda hicho.

Vile vile, Bw Dima alisema uamuzi wa kulipa wakulima kwa wakati au hata mapema kumewapa motisha wakuzaji ambao walikuwa wameasi kilimo hicho na sasa wamekirejelea.

“Sasa tunapokea tani 20,000 za miwa kila wiki, idadi ambayo ni ya juu kuliko zamani,” akaongeza.

Hata hivyo, kikwazo kikuu kwa Sony Sugar deni la Sh800 milioni la wafanyakazi ambalo limerundikana kwa miezi 16 iliyopita.

Mvua, joto na baridi zitazidi katika maeneo tofauti nchini Kenya

Wakenya wameshauriwa kujiandaa kwa mvua kubwa na baridi kali katika baadhi ya maeneo katika kipindi cha siku tano zijazo. Picha| Hisani

IDARA ya Utabiri wa Hali ya Hewa Kenya  imewatahadharisha Wakenya kujiandaa kwa mvua  mara  kwa mara  hadi Jumanne, Desemba 24.

Katika ushauri wake, idara ya utabiri wa hali ya hewa ilitangaza kuwa Nyanda za Juu Mashariki na Magharibi mwa Bonde la Ufa, Bonde la Ziwa Victoria, Bonde la Ufa la Kati na Kusini, Nyanda za Juu Kusini Mashariki na Pwani zitapata mvua.

Kaunti za Nyanda za Juu Mashariki za Nyandarua, Laikipia, Nyeri, Kirinyaga, Murang’a, Kiambu, Meru, Embu, Tharaka Nithi na Nairobi zinatarajiwa kupata mvua ya wastani hadi kubwa katika muda wa siku tano kuanzia Jumamosi Desemba 21.

Kulingana na  idara hiyo utabiri umeonyesha kuwa kaunti za Nyanda za Juu Mashariki zitapata mvua  kiasi  asubuhi lakini itanyesha sana mchana.

Kaunti za Siaya, Kisumu, Homabay, Migori, Kisii, Nyamira, Trans Nzoia, Baringo, Uasin Gishu, Elgeyo-Marakwet na Nandi zinatarajiwa kupokea mvua zaidi ya wastani katika kipindi cha siku tano zijazo.

Mvua katika kaunti zilizotajwa hapo juu ilitarajiwa hasa alasiri na itaambatana na radi huku idara ya utabiri wa hali ya anga ikiwataka wakazi kuwa macho dhidi ya mafuriko ambayo yanaweza kutokea.

Kaunti zingine ambazo zilitarajiwa kukumbwa na hali sawa ya anga ni pamoja na Nakuru, Narok, Kericho, Bomet, Kakamega, Vihiga, Bungoma, Busia na Kaunti ya Pokot Magharibi.

Kaunti za pwani za Mombasa, Kilifi, Lamu na Kwale pamoja na sehemu za pwani za Kaunti ya Tana River zilitarajiwa kupata mvua ndogo asubuhi na alasiri.

Huku maeneo kadhaa nchini yakitarajiwa kukumbwa na mvua wikendi hii, idara ya utabiri wa hali ya anga pia iliwatahadharisha wakazi wa Kaunti za Nyandarua, Laikipia, Nyeri, Kirinyaga, Murang’a, Kiambu, Meru, Embu, Tharaka na Nairobi kuhusu majira ya baridi kali usiku.

Kulingana na idara hiyo, kaunti hizo zilitarajiwa kukumbwa na baridi kali kwa siku tano zijazo. Halijoto ya usiku inatarajiwa kushuka hadi nyusi 11°C.

Vile vile, viwango vya juu vya joto mchana vinatarajiwa katika kaunti za Siaya, Kisumu, Homabay, Migori, Kisii, Nyamira, Trans Nzoia, Baringo, Uasin Gishu, Elgeyo-Marakwet, Nandi, Nakuru, Narok, Kericho, Bomet na Kakamega.

Halijoto  mchana katika maeneo haya inatarajiwa kuzidi nyusi 30°C huku kaunti za pwani za Mombasa, Kilifi, Lamu na Kwale zikitabiriwa kukumbwa na kiwango sawa cha joto.

Saba wafariki katika ajali ya magari sita na pikipiki eneo la Mai Mahiu nchini Kenya

Mabaki ya magari yaliyohusika katika ajali eneo la Duka Moja, katika barabara ya Nairobi-Mai Mahiu

WATU saba wameaga dunia katika ajali iliyohusisha magari sita na pikipiki eneo la Mai Mahiu katika barabara ya Narok – Nairobi.

Kulingana na polisi, magari sita yalihusika katika ajali hiyo ya saa nne asubuhi Jumatatu.

Mabaki ya magari yaliyohusika katika ajali Mai Mahiu.

Kaimu Kamanda wa Kaunti ya Narok John Momanyi hakubainisha moja kwa moja idadi ya waliojeruhiwa.

“Ajali ilitokea wakati trela iliyokuwa ikisafiri kutoka Narok kuelekea Mai Mahiu ilipasuka gurudumu,” akasema Bw Momanyi.

Alisema trela hiyo iligonga gari aina ya Toyota Premio na basi la kampuni ya Ena Coach.

“Abiria watatu wa matatu walifariki papo hapo eneo la Duka Moja na Nairegia Enkare,” akafichua Bw Momanyi.

Wawili waliosafiri katika Toyota Prado walifariki papo hapo huku msafiri wa tatu akiaga dunia akipokea matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Narok.

“Trela ya pili iligonga pikipiki na kuua abiria wawili papo hapo,” Bw Momanyi akaeleza.

Moja ya trela lililohusika katika ajali mbaya Mai Mahiu Desemba 23, 2024.

Magari yote yaliyohusika katika ajali pamoja na pikipiki zilipelekwa katika Kituo cha Polisi cha Ntulele.

Hadi wakati wa kuchapishwa kwa habari hii, majeruhi, ambao idadi yao haikubainika, walisafirishwa hadi Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Narok kwa matibabu.

Ajali hiyo ilisababisha msongamano mkubwa wa magari kwa saa kadhaa huku polisi wakiwa na kazi ngumu kuondoa magari yaliyoharibika.

Bw Momanyi aliomba madereva wawe waangalifu na wafuate sheria za barabarani kuepuka ajali hasaa msimu wa Krismasi na mwaka mpya.

KIPENGA CHA MICHEZO

‘Kila kitu ni kigumu’ – Amorim atafuta majibu Man Utd

.
Maelezo ya picha,Amorim

Je, maisha ndani ya Manchester United yanaweza kuwa ya kukatisha tamaa zaidi?

Wametoka tu kufungwa 3-0 nyumbani na klbau ndogo ya Bournemouth kama alivyoeleza mmiliki wa Cherries Bill Foley, kwa msimu wa pili unaoendelea, matokeo ambayo yanamaanisha kuwa watahudumia Krismasi wakiwa nafasi ya 13 kwenye jedwali. Ni mara ya kwanza kuwa katika nusu ya mwisho katika hatua hii tangu ufanisi wa klabu hiyo uanze .

Mashabiki wao – ambao waliizomea timu ya Ruben Amorim kwenye kipenga cha mwisho – wamekasirishwa sana na kupanda kwa bei ya tikiti hadi pauni 66 bila makubaliano hatua ambayo imewafanya kuungana na wafuasi wenzao wa Liverpool kuandamana wakati timu hizo mbili zitapokutana Anfield tarehe 5 Januari.

Wakati Amorim alipokuwa akiambia vyombo vya habari alihisi mashabiki “wamechoka” katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya mechi, uvujaji kutoka kwenye dari ulisababisha maji kuwatiririka waandishi wa habari waliokuwa mstari wa mbele, na kumlazimu mmoja wao kusonga mbele.

Lakini kwa Amorim, msimao wa United katika jedwali si jambo la mzaha. Beki Lisandro Martinez aliiambia Mechi Bora ya Siku hali ya uwanjani inamfanya “akasirike”. Bosi wake lazima atafute majibu.

“Kwa wakati huu, kila kitu ni kigumu sana,” Amorim alisema. “Katika klabu kama Manchester United, kupoteza 3-0 nyumbani, ni ngumu sana kwa kila mtu.

“Kwa kweli mashabiki wamekatishwa tamaa na wamechoka. Unaweza kuhisi katika uwanja.

.
Maelezo ya picha,Wachezaji wa Man United wakiwa na kocha wao Reuben Amorim

Ikiwa kuna tofauti kubwa iliyoletwa na Mreno huyo kwa muda mfupi tangu achukue nafasi ya Erik ten Hag mwezi uliopita, ni kwamba United wana udhibiti zaidi wa mpira katika mechi.

Takwimu zao za umiliki ziko juu 60% leo. United walikuwa na mashabulizi mengi na mashuti mengi yaliyolenga lango kuliko Bournemouth. Lakini walipoteza, vibaya

Kwa mara ya pili pekee katika historia yao – nyingine ikiwa dhidi ya Burnley katika miaka ya 1960 – wamepoteza mechi mfululizo za nyumbani dhidi ya wapinzani kwa tofauti ya mabao matatu.

Ingesaidia sana ikiwa hawangeendelea kuruhusu mabao kwenye ‘set pieces’.

Ilitokea mara mbili , dhidi ya Arsenal mapema mwezi huu na dhidi ya Nottingham Forest katika mchezo wao wa mwisho wa nyumbani. Wakiwa Tottenham siku ya Alhamisi, Son Heung-min alifunga bao la moja kwa moja kutoka kwa kona.

Wote hawakuwa chini ya uangalizi wa Amorim, lakini United sasa wameruhusu mabao 17 kutoka kwa set piece kwenye Premier League mwaka huu, ikiwa idadi kubwa zaidi katika mwaka mmoja wa kalenda kwenye mashindano.

Makosa ya hivi majuzi yanazua swali, je, kocha Carlos Fernandes, ambaye aliandamana na Amorim kutoka Sporting, anafanya nini hasa?

Sio kwamba Amorim anagawanya lawama.

“Jukumu ni juu yangu, sio Carlos,” alisema.

“Sisi ni timu katika wakati mzuri na wakati mbaya. Tuna njia ya kufanya mambo. Tunalifanyia kazi hilo na tunaenda kuboresha hilo. Lakini hatukupoteza kwa sababu ya kuweka vipande. Tumepoteza kwa sababu tumeunda. nafasi zaidi na hatukufunga.”

Akizungumza na Mechi ya Siku, Martinez aliiweka kwa uwazi zaidi.

“Tuna hasira sana na hali ya aina hii,” alisema beki huyo wa Argentina. “Lazima tufanye kazi zaidi katika ‘set pieces’ haswa.

“Ninaamini sana katika timu hii na wachezajii. Ikiwa hawatafunga bao lao la kwanza kutoka kwa seti piece basi ni mchezo tofauti kabisa.”

Amorim inatatizwa na ukosefu wa ubora.

Mreno huyo alimwamini Tyrell Malacia katika nafasi ya beki wa kushoto, lakini alimtoa Mholanzi huyo wakati wa mapumziko baada ya kumtazama akiutoa mpira kwa rahisi mara nyingi na hakutoa chochote kwenda mbele.

Diogo Dalot alibadilisha safu yake, lakini tishio lake la bao moja lilikosa imani. Noussair Mazraoui alikwenda kwa beki wa kushoto kutoka nafasi yake katika safu ya ulinzi ya watu watatu, lakini alimchezea visivyo Justin Kluivert ambaye alimruhusu fowadi huyo kufunga bao la pili la Bournemouth kutoka kwa mkwaju wa penalti.

Mechi ikiendelea , nahodha Bruno Fernandes pekee ndiye aliyekuwa hatari kwa lango la Bournemouth, huku Marcus Rashford akiwekwa benchi kwa mechi ya tatu mfululizo, ingawa alikuwa Old Trafford kutazama matukio ya huzuni yanayoendelea.

“Inategemea, tutaona,” alisema Amorim alipoulizwa kama fowadi huyo wa Uingereza anaweza kugombania nafasi yake siku ya Boxing Day dhidi ya Wolves.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment