Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Rais mteule Donald Trump amepinga makubaliano ya bajeti kati ya Republican na Democrats siku ya Jumatano ili kuepusha kuzorota kwa bajeti ya serikali, ambayo inaweza kutokea mapema siku ya Ijumaa jioni.
Donald Trump ameelezea upinzani wake kwa makubaliano ya bajeti yaliyojadiliwa katika Bunge la Marekani kati ya viongozi waliochaguliwa wa Republican na Democratic siku ya Jumatano, Desemba 18, na hivyo kuibua zaidi hali ya kudhoofika kwa serikali ya shirikisho kufikia makataa ya Ijumaa jioni.
Mwanachama wa Republican, ambaye atarejea Ikulu mnamo Januari 20, alifurahia uchapishaji kwenye jukwaa lake la Truth Social kwamba mswada huu “wa kipuuzi na wa gharama isiyo ya kawaida” “unakufa haraka”.
Katika taarifa ya pamoja na makamu wake wa baadaye J.D. Vance, pia alithibitisha kwamba makubaliano yoyote kwa Wademocrats ni “usaliti wa nchi yetu” na kwamba Warepublicans hawapaswi kutishwa na tishio la kuzorota kwa taifa hili, maarufu ” shutdown”.
Kabla ya hapo, mtu tajiri zaidi duniani, Elon Musk, alikuwa tayari ameshambulia makubaliano hayo katika mfululizo wa machapisho mengi siku ya Jumatano kwenye mtandao wake wa kijamii akifanya kampeni pamoja na Donald Trump na aliteuliwa na kiongozi huyo kuongoza tume ya kupunguza matumizi ya fedha za umma.
“Afisa yeyote aliyechaguliwa katika Baraza au Seneti ambaye anapigia kura mradi huu wa kashfa wa matumizi anastahili kupoteza nafasi yake katika miaka miwili,” pia amesema mmiliki wa Tesla na SpaceX. Kwa utawala wa Biden, kukosekana kwa makubaliano ya bajeti kunahatarisha “kuwadhuru Wamarekani wanaofanya kazi kwa bidii” na “kuunda ukosefu wa utulivu”.
“Warepublicans wanapaswa kuacha kucheza michezo ya kisiasa,” msemaji wa White House Karine Jean-Pierre amesema katika taarifa.
Kufungia mishahara ya baadhi ya watumishi wa umma na mafao kadhaa ya kijamii
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mike Johnson kutoka chama cha Republican, aliwasilisha makubaliano haya ya bajeti ya zaidi ya kurasa 1,500 siku ya Jumanne. Ilijadiliwa na Wademocrats, ilijumuisha, kati ya mambo mengine, zaidi ya dola bilioni 100 za msaada dhidi ya majanga ya asili iliyoombwa na Joe Biden.
Nakala hiyo ilifanya iwezekane kufadhili serikali ya shirikisho hadi katikati ya mwezi Machi na hivyo kuepuka “kuzorota” kabla ya saa ya kutisha ya usiku wa manane sikuya Ijumaa kuamkia Jumamosi.
Hali isiyopendeza sana, haswa Krismasi inapokaribia. Mara tu makubaliano yaliyojadiliwa katika Congress yalipochapishwa, maafisa waliochaguliwa wanaomuunga mkono Donald Trump – wafuasi wa hali ya chini ya serikali ya shirikisho – wamepinga kwa kile walichokiona kuwa matumizi yasiyo ya busara.
Mswada huu unawakilisha “zawadi ya Krismasi upande wa kushoto”, amesema afisa mteule Russell Fry. Kiongozi wa chama cha Democrats katika Baraza la Wawakilishi, Hakeem Jeffries, ametangaza kwamba kwa upinzani huu kutoka kwa Donald Trump, maafisa waliochaguliwa wa Republican “wamepokea amri ya kudhoofisha serikali” na “kuwafanya wafanyakazi wa Marejkani kuteseka kama wanavyodai kustahimili”.
Kiwango cha deni ambacho kinamsumbua Donald Trump
Wademocrats wengine wameshtumu ushawishi wa Elon Musk kwa uamuzi wa rais mteule. “Usiku wa leo, Donald Trump na maafisa waliochaguliwa wa Republican wameinamisha vichwa vyao kwa rais mteule halisi, Elon Musk,” amekosoa afisa aliyechaguliwa wa New York Nydia Velazquez Hatua zinazofuata za kuzuia “kuzorota kwa serikali” sasa hazina uhakika.
Kwa baadhi ya maafisa waliochaguliwa wa Trumpist, mswada mpya unaotoa matumizi madogo zaidi unapaswa kuwasilishwa kwa haraka kwa Bunge la Congress, suluhisho ambalo rais mteule huzingatia, lakini sio bila masharti. KwenyeTruth Social, Donald Trump amehakikisha kwamba nakala kama hii haitakuwa na manufaa ikiwa haitaambatana na ongezeko la kiwango cha deni.
Marekani ina umahususi wa kukabiliana mara kwa mara na kikwazo cha kisheria kuhusu uwezo wake wa mikopo: kiwango hiki cha juu cha deni, ambacho lazima kitozwe rasmi au kusimamishwa na BungeCongress.
Muda wa kusimamishwa ulioamuliwa mnamo mwaka 2023 utaisha mwanzoni mwa mwezi Januari na Marekani inapaswa kufikia kiwango cha juu mnamo mwezi Juni.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.