Canada: Mgomo waitishwa kupinga mageuzi yasiyokoma katika sheria za uhamiaji

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wahamiaji ambayo inaadhimishwa siku ya Jumatano, Desemba 18, mashirika kadhaa ya Quebec yanaitisha mgomo kupinga mageuzi yasiyokoma katika sheria za uhamiaji. Pia wanakusudia kushutumu kurefushwa kwa muda wa kushughulikia faili za wanaotafuta hifadhi mbele ya mahakama ya utawala wakati ambapo idadi yao inaongezeka kwa kasi – iliongezeka maradufu mwaka jana. Hali inashtumiwa na ripota maalum wa zamani wa Umoja wa Mataifa kuhusu wahamiaji.

Kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa na Ottawa, serikali ya Quebec tayari imeomba mara kadhaa kuweza kusimamia uhamiaji kwa kujitegemea, daima bila mafanikio. Hapa, waandamanaji wanadai haki zaidi kwa wahamiaji, wakimbizi na wahamiaji, pamoja na kuhalalishwa kwa wahamiaji wasio na vibali mjini Montreal, Machi 16, 2024.
Kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa na Ottawa, serikali ya Quebec tayari imeomba mara kadhaa kuweza kusimamia uhamiaji kwa kujitegemea, daima bila mafanikio. Hapa, waandamanaji wanadai haki zaidi kwa wahamiaji, wakimbizi na wahamiaji, pamoja na kuhalalishwa kwa wahamiaji wasio na vibali mjini Montreal, Machi 16, 2024. © Mathiew Leiser / AFP

“Wahamiaji hawalalamiki. Wahamiaji hawawezi kulalamika kwa sababu wanaogopa mamlaka. ” Sasa profesa wa sheria katika Chuo Kikuu cha McGill huko Montreal, François Crépeau anashutumu kutochukua hatua kwa serikali ya Canada kuhakikisha kwamba maombi ya hifadhi yanashughulikiwa ndani ya muda muafaka.

Kwa sasa, inachukua miaka miwili hadi mitatu kupata hadhi ya ukimbizi inayotolewa na makamishna wa mahakama ya utawala, muda ambao unaendelea kuongezeka. “Tunapaswa kuwekeza. Na kwa hivyo tunapaswa kuongeza zaidi idadi ya makamishna kwa sababu idadi haiongezeki kulingana na mahitaji kama tunavyofanya kwa raia,” anasema François Crépeau.

Alipowasili Canada miaka mitano iliyopita, mzaliwa huyu wa Haiti anapata ugumu kukabiliana na wakati uliopotea katika msururu wa utawala ili kupata haki ya hifadhi: “Kuna nyakati ambapo inanizuia kulala. Kwenye treni, ili kwenda kazini, nililia kwa sababu sijui la kufanya. Hata mwanasheria wangu, wakati fulani nilipotaka kushauriana naye, sikuweza kumfikia. Hili ni tatizo. “

Akiwa ameajiriwa katika nyumba ya kustaafu, mama huyu bado hajui kama ataweza kuendelea kuishi Canada. Hasa kwa vile wanaotafuta hifadhi, ambao mara nyingi hutajwa na mamlaka za kisiasa kama sababu ya matatizo ya kijamii, hawajisikii kwamba wako huru nchini.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment