Tetesi za Soka Ulaya: Arsenal & Chelsea wanamtaka Isak
Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Saa 9 zilizopita
Chelsea na Arsenal wanamtaka mshambuliaji wa Newcastle Alexander Isak, Manchester United yaarifiwa kuhusu hali ya kandarasi ya Alphonso Davies Bayern Munich na Graham Potter auliziwa na Wolves na West Ham.
Arsenal na Chelsea zinamtafuta mshambuliaji na klabu hizo mbili za London zina orodha sawa ya wachezaji wanaowataka, ambayo ni pamoja na mshambuliaji wa Newcastle United na Uswidi Alexander Isak, 25. (Caught Offside)
Manchester United pia imefanya usajili wa mshambuliaji kuwa kipaumbele chake katika uhamisho la Januari. (Mirror)
Bayern Munich wanajiandaa kumuongeza mkataba wa mchezaji wao wa kimataifa wa Canada Alphonso Davies, huku Manchester United wakifahamu kuwa beki huyo mwenye umri wa miaka 24 huenda akasaini mkataba mpya licha ya kumtaka. (Floran Plettenberg, Sky Germany)

Bayern Munich kumuongeza mkatabamchezaji wao wa kimataifa wa Canada Alphonso Davies
Manchester United wako nyuma ya Chelsea katika kinyang’anyiro cha kumsajili beki wa Lecce raia wa Denmark Patrick Dorgu. (Team Talk)
Kocha wa zamani wa Chelsea na Brighton Graham Potter ameuliziwa na klabu za Wolves na West Ham. (Sportsport)
Kocha wa zamani wa Borussia Dourtmund Edin Terzic hatakuwa mkufunzi mpya wa West Ham ikiwa Lopetegui ataondolewa kwenye nafasi yake, lakini mkufunzi wa zamani wa Denmark Kasper Hjulmand yuko kwenye kinyang’anyiro. (Florian Plettenberg)
Kocha wa zamani wa West Ham David Moyes ni miongoni mwa wanaowania nafasi ya kazi katika klabu ya Wolves iwapo Gary O’Neil atafukuzwa (Telegraph – usajili unahitajika)
Liverpool wanawasiliana na Bayer Leverkusen kuhusu uhamisho wa beki wa Uholanzi Jeremie Frimpong, 23. (Caught Offside)
Manchester City itamruhusu kiungo wa Ubelgiji Kevin De Bruyne, 33, kujiunga na moja ya vilabu dada vya City Football Group atakapoondoka kwenye kikosi cha Ligi ya Primia. (Telegraph – usajili unahitajika)
Lakini Inter Miami ya David Beckham imemfanya De Bruyne kuwa shabaha yao kuu ya uhamisho. (Mirror)
Mshambuliaji wa Everton na Guinea-Bissau Beto, 26, na kiungo wa Mali Abdoulaye Doucoure, 31, wanasakwa na klabu ya Roma. (Gazzetta dello Sport kupitia Football Italia)

Liverpool wana uhakika mlinzi wa Ufaransa Ibrahima Konate, 25, atasaini mkataba mpya na klabu hiyo huku mazungumzo yakiendelea kuhusu mkataba mpya. (Fabrizio Romano)
Juventus na Marseille wana nia ya kumsajili beki wa Chelsea mwenye umri wa miaka 23 Mfaransa Benoit Badiashile. (Caught Offside)
Chelsea imefanya mawasiliano na klabu ya Benfica kuhusu mpango wa kumsajili beki wa Ureno Tomas Araujo, 22, huku klabu hiyo ya London ikiwa tayari kumruhusu mlinzi wa Ufaransa Axel Disasi, 26, kuondoka mwezi Januari. (Team Talk )

Mustakabali wa Fabio Vieira wa Arsenal katika klabu hiyo uko mashakani huku The Gunners wakiwa tayari kupokea ofa ya kumuuza kiungo huyo wa kati Mreno mwenye umri wa miaka 24, ambaye kwa sasa yuko Porto kwa mkopo. (Daily Mail – usajili unahitajika)
Mkurugenzi wa kandanda wa Barcelona Deco amekutana na wawakilishi wa beki wa Ujerumani Jonathan Tah, 28, ambaye mkataba wake katika klabu ya Bayer Leverkusen unamalizika msimu ujao. (Mundo Deportivo – kwa Kihispania)
Shabiki wa Uganda apigwa risasi akisherehekea Arsenal kuifunga Manchester United

Shabiki wa klabu ya Arsenal ya Uingereza, ambaye alikuwa akishangilia ushindi wa timu hiyo dhidi ya Manchester United, anadaiwa kupigwa risasi na mlinzi mmoja nchini Uganda.
Shabiki mwingine alijeruhiwa wakati mlinzi huyo alipoufyatulia risasi umati mkubwa wa wafuasi waliokuwa wakishangilia katika mgahawa mmoja katika mji wa Lukaya katikati mwa Uganda, yapata kilomita 100 kutoka mji mkuu Kampala.
Tukio hilo lilifanyika kuelekea mwisho wa mechi, ambayo Arsenal ilishinda 2-0.
Mwandishi wa habari wa eneo hilo aliambia BBC kwamba meneja wa jengo hilo alikasirishwa na kelele ambazo wafuasi hao waliokuwa wakishangilia walikuwa wakipiga na akamwomba mlinzi huyo kuingilia kati.
Hatahivyo mashabiki hawakuzingatia onyo la kunyamaza.
Walioshuhudia tukio hilo walimweleza mwandishi wa habari hizi, Farish Magembe kuwa mmiliki alizima umeme katika mgahawa huo hali iliyowakasirisha mashabiki ambao walijibu kwa kupiga kelele zaidi.
Hapo ndipo mlinzi huyo anadaiwa kufyatua risasi kadhaa.
Mwathiriwa aliyetambulika kwa jina la John Ssenyonga mwenye umri wa miaka 30 alifariki katika eneo la tukio. Shabiki mwingine wa muda mrefu wa Arsenal, Lawrence Mugejera, alipelekwa hospitali kwa matibabu.
Mlinzi na meneja wa jengo hilo wamekuwa mafichoni baada ya tukio, huku polisi wakiwatafuta.
Msemaji wa Jeshi la Polisi mkoani, Twaha Kasirye, alinukuliwa na gazeti la Daily Monitor akisema walipata bunduki katika eneo la tukio.
“Tunalaani tukio hilo na tunaomba yeyote mwenye taarifa zinazoweza kusaidia polisi kumfikisha mtuhumiwa huyo ili aweze kuzungumza,” alisema.
Pia aliwataka mashabiki kudhibiti msisimko wao.
Mvutano na vurugu za kusikitisha zinazotokana na matokeo ya mechi za soka hasa baina ya klabu za Uingereza si jambo la kawaida katika nchi hiyo ambayo Ligi Kuu ya England inafuatiliwa kwa karibu.
Mwezi Oktoba, shabiki wa Arsenal alimdunga kisu shabiki wa Manchester United baada ya wawili hao kuzozana kuhusu matokeo ya pambano kati ya Arsenal na Liverpool.
Januari mwaka jana, diwani mmoja kijana alifariki kutokana na majeraha ya kuchomwa visu mjini Kampala baada ya kuingilia kati pambano lililotokea baada ya Arsenal kushindwa na Manchester City.
Wiki moja tu kabla ya hapo, shabiki wa Arsenal alikuwa amepigwa na kifaa kutu hadi kufa huko Adjumani, katika wilaya ya Nile Magharibi.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.