Liberia: Aliyekuwa mbabe wa kivita Prince Johnson afariki dunia

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Nchini Liberia, Seneta Prince Johnson, mwanasiasa mwenye utata katika siasa za kitaifa, amefariki akiwa na umri wa miaka 72, vyombo vya habari nchini humo vinaripoti. Chanzo cha kifo chake hakijathibitishwa. Kiongozi wa zamani wa waasi na seneta tangu mwaka 2006, amekuwa akiwakilisha kaunti ya Nimba, kituo chake cha uchaguzi, ambapo alirejea siku ya Jumatano kabla ya kufariki.

Aliyekuwa mbabe wa kivita nchini Liberia, Prince Johnson akihutubia wafuasi wake mnamo Novemba 2011.
Aliyekuwa mbabe wa kivita nchini Liberia, Prince Johnson akihutubia wafuasi wake mnamo Novemba 2011. AFP – ISSOUF SANOGO

Johnson alikuwa na jukumu muhimu katika uchaguzi wa rais wa sasa Joseph Boakai, kutokana na ushawishi wake huko Nimba, ambapo mkuu wa sasa wa nchi alipata zaidi ya 74% ya kura. Kifo cha Johnson kinamaliza urithi ulioendana na jukumu lake katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na ushawishi wake wa kisiasa.

Aliyekuwa mbabe wa kivita wa Liberia Prince Johnson amefariki Novemba 28, 2024 akiwa na umri wa miaka 72. Baraza la Seneti, ambalo alikuwa mwanachama wake, na chama chake cha Movement for Democracy and Reconstruction, vinathibitisha kwamba amefariki katika hospitali ya Hope for Women huko Paynesville, kitongoji cha Monrovia. Kwa sasa, sababu za kifo chake cha ghafla bado hazijajulikana. Ni mtu mwenye utata sana katika historia ya Liberia ambaye ameaga dunia.

Prince Yormie Johnson kwa kweli anajulikana zaidi kwa jukumu lake kuu katika vita vya kwanza vya wenyewe kwa wenyewe vilivyozuka mwaka wa 1989. Wakati huo, mbabe huyu wa kivita aliunga mkono uasi ulioongozwa na Charles Taylor (1997-2003), rais wa baadaye wa Liberia. Ilikuwa mwaka wa 1990 ambapo sifa ya Prince Johnson ya ukatili wa hali ya juu ilionekana.

Akiwa na watu wake, walimkamata rais wa wakati huo, Samuel Doe, wakamtesa mbele ya kamera. Mlolongo huu mbaya unamwonyesha Samuel Doe akiwa amepiga magoti, akiomba aachiwe hai, asiuawe, huku Johnson akiendesha mahojiano huku akinywa bia. Samuel Doe kisha akauawa na maiti yake kuonyeshwa katika mitaa ya Monrovia.

Kuachana na Charles Taylor, Prince Johnson alienda uhamishoni nchini Nigeria, ambako alijiunga na Ukristo na kuwa mchungaji.

Alirejea Liberia baada ya kuondoka kwa Rais Taylor, alianza mpito wake wa kisiasa na, mwaka wa 2005, alichaguliwa seneta kutoka Kaunti ya Nimba, eneo la nyumbani kwake. Kiti ambacho amekishikilia hadi kifo chake.

Akishika nafasi ya 3 katika uchaguzi wa rais wa 2011, Prince Johnson alikua mdau mkuu wa kisiasa, na hivyo kufurahia hali ya kutokujali na kujumuisha vitisho vya vita na changamoto za amani nchini Liberia.

Mnamo mwaka 2008, kwenye RFI, alikiri kushiriki katika mauaji ya rais wa Burkina Faso Thomas Sankara mnamo 1987, kwa faida ya Blaise Compaoré ambaye anlichukua madaraka.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment