DRC na Rwanda zapiga hatua mbele katika mchakato wa amani

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda, ambazo zilitia saini makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano mapema mwezi Agosti, zimeidhinisha waraka “muhimu” kwa ajili ya kuendeleza mchakato wa amani mashariki mwa DRC, diplomasia ya Angola imesema.

Kutoka kushoto kwenda kulia, Mawaziri wa Mambo ya Nje wa DRC (Thérèse Kayikwamba Wagner), wa Angola (Tete António) na wa Rwanda (Olivier Nduhungirehe) Novemba 5, 2024 huko Goma wakati wa uzinduzi wa "tume ya mseto" (MVA-R).
Kutoka kushoto kwenda kulia, Mawaziri wa Mambo ya Nje wa DRC (Thérèse Kayikwamba Wagner), wa Angola (Tete António) na wa Rwanda (Olivier Nduhungirehe) Novemba 5, 2024 huko Goma wakati wa uzinduzi wa “tume ya mseto” (MVA-R). © Héritier Baraka/RFI

Kanda hii inayokumbwa na misukosuko tangu mwisho wa mwaka 2021 na kuibuka tena kwa M23, kundi la waasi linaloungwa mkono na Kigali na jeshi lake ambalo liliteka maeneo makubwa ya ardhi kwa gharama ya Wanajeshi wa Kongo (FARDC) na wanamgambo wanaounga mkono setrikali ya Kinshasa. Mwanzoni mwa mwezi wa Agosti, Angola, mpatanishi aliyeteuliwa na Umoja wa Afrika, alipata saini ya usitishaji mapigano, lakini M23 inaendelea kufanya mashambulizi katika maeneo mbalimbali Mashariki mwa DRC.

Siku ya Jumatatu, mawaziri wa mambo ya nje wa DRC na Rwanda “walichunguza na kuidhinisha Dhana ya Operesheni (CONOPs), chombo muhimu”, kinachopaswa kuweka masharti ya uwezekano wa kutoshirikishwa kwa wanajeshi wa Rwanda waliopo kwenye eneo la Kongo, imetangaza Wizara ya Mambo ya Nje ya Angola, katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotumwa kwa shirika la habari la AFP.

Hati hii ya CONOPS, inayotumika katika uwanja wa kijeshi kuweka ratiba ya operesheni na mpangilio wa uwezo wake, “itaongoza utekelezaji wa mpango ulioainishwa” unaopaswa kuleta amani kati ya nchi hizo mbili jirani, kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari ambayo haitoi maelezo yoyote juu ya masharti yaliyozingatiwa.

Toleo la kwanza la “mpango huu uliooanishwa” wa mwezi wa Agosti, uliowekwa kama sharti la kuondoka kwa wanajeshi wa Rwanda kwenye ardhi ya DRC, kuangamizwa kwa waasi wa Kihutu kutoka Rwanda (FDLR), kundi lenye silaha lililoundwa na viongozi wa zamani wa Wahutu waliohusika katika mauaji ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, yaliyoonyeshwa na Kigali kama tishio kwa mipaka yake. Kwa sasa FDLR inapigana katika kambi ya serikali dhidi ya M23, kama wanamgambo walioanzishwa mashariki mwa DRC.

Hakuna maelezo yoyote ambayo yamewasilishwa na mamlaka ya Angola kwa masharti ya CONOPS, kama ilivyoidhinishwa na pande zote mbili. Licha ya ukiukaji wa usitishaji mapigano, DRC na Rwanda zinadumisha mazungumzo kupitia Angola. Majirani hao wawili walitangaza mwanzoni mwa mwezi wa Novemba kuteuliwa kwa kamati ya kufuatilia ukiukaji wa usitishaji mapigano, inayoongozwa na Angola, na kujumuisha wawakilishi kutoka DRC na Rwanda.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment