Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Kituo cha udhibiti wa magonjwa barani Afrika, CDC, kimesema kinatafuta hakikisho toka kwa utawala wa Rais mteule wa Marekani Donald Trump, kuhusu ikiwa utatimiza ahadi yake ya ufadhili na chanjo ya mpox iliyoahidiwa na mtangulizi wake.
Mwezi Septemba, Rais Joe Biden aliahidi kutoa dola milioni 500 na dozi milioni 1 za chanjo katika mpango wa kukabiliana na mlipuko wa mpox barani Afrika.
Aidha wakati huu wagonjwa wa mpox wakiongezeka na maambukizo kuanza kupungua barani Afrika, wafadhili nao wamepunguza kasi ya kutumiza ahadi za kifedha na chanjo, amesema mkurugenzi wa CDC.

Alipoulizwa kama ushindi wa Trump unaweza kuathiri uungaji mkono wa Marekani katika kuchangia huduma za afya barani Afrika, Mkurugenzi wa CDC John Kaseya alisema ataufuatilia utawala mpya kutimiza ahadi zilizopo.
Hivi majuzi Trump alisema atamruhusu mwanaharakati anayepinga masuala ya chanjo Robert F. Kennedy Jr. kufanya maamuzi kuhusu sera ya afya ya Marekani.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.