Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Viongozi wa dunia wameendelea kumpongeza rais mteule wa Marekani, Donald Trump baada ya ushindi alioupata dhidi ya Kamala Harris, viongozi wengi wa Ulaya wakiwa wa kwanza kufanya hivyo.

Rais wa Ufaransa ni miongoni mwa viongozi wa kwanza, waliompongeza Trump kwa ushindi alioupata, kupitia ujumbe aliouandika kwenye mitandao yake ya kijamii.
Macron amemwambia Trump kuwa yuko tayari kuendelea kufanya kazi naye kwa kuheshimiana kama ilivyokuwa miaka minne aliyowahi kuwa madarakani.

Mkuu wa Tume ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen hakuachwa nyuma kumpongeza Trump kupitia ukurasa wake wa X, akimwambia kuwa EU na Marekani zitaendelea kushrikiana na kuwaunganisha watu.
China kupitia Wizara ya Mambo ya nje, imesema Beijing, inatumai kuwa kutakuwa na ushirikiano wa amani na Washington DC na kila upande, utanufaika.

Naye Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu amesema, ushindi wa Trump ni mwanzo mpya kati ya nchi yake na Marekani na kuelezea ushindi wake kama wa kihistoria.
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi amemwambia Trump kuwa anatumai uongozi wake utasaidia kurejesha amani Mashariki ya Kati na uhusiano kati ya mataifa hayo mawili yataimarika, huku rais wa mamlaka ya Palestina, Mahamud Abbas akisema anatumai Trump atasaidia kupatikana kwa taifa la Kipalestina.

Viongozi wa mataifa ya Afrika, wakiongozwa na rais wa Nigeria Bola Tinubu, Emmerson Mnangagwa, Evariste Ndayishimiye na Felix Tshisekedi ni miongoni mwa marais waliompongeza Trump kwa ushindi.
Rais wa #China #XiJinping amempongeza rais mteule wa Marekani #DonaldTrump na kutoa wito wa kuwepo kwa ushirikiano wa kudumu kati ya mataifa hayo mawili.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.