Maumivu 8 Ya Moyo Yalivyoharibu Maisha Ya Watu Wengi.

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Unataka Kupona MAUMIVU ya MOYO?…

i. Kutoamini watu wanaopaswa kuaminika.

ii. Kukata tamaa

iii. Kutojipenda.

iv. Kutoamini kwenye uwezo wako.

v. Kukosa Uimara wa kihisia

vi. Kufa kwa Hisia Muhimu.

vii. Mgonjwa.

viii.Kuzeeka.

Katika Makala Hii Tutazungumzia…

– Kutojipenda.

Kuna watu ambao wakipitia maumivu, hawawezi kujipenda tena.

Si unakumbuka jinsi ambavyo zamani ulikuwa ni mtu unayejipenda sana.

Unavaa vizuri.

Unapaka manukato (perfume).

Na hauachi kwenda saluni mara kwa mara.

Baada ya maumivu kutokea, angalia jinsi unavyopuuzia utanashati wako.

Haujali tena mwonekano wako.

Mtu akiwa kwenye maumivu huwa hajali mwonekano wake.

Hajali tena kama anamechisha rangi za nguo zake au la.

Anaweza kutoka hajachana nywele.

Au hata hajapaka mafuta.

Ni mtu ambaye hajali hata kula yake.

Anaweza kukaa na njaa kwa siku nzima bila sababu yoyote ile.

Maumivu huwafanya watu ambao walikuwa wanang’ara kugeuka na kuwa watu wasioweza kupendeza tena.

Kama unataka kujifunza Mbinu Za Kupona MAUMIVU ya MOYO…

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment