Mbinu 5 Za Kuondoa Migogoro Inayosababishwa na Pesa Kwenye Ndoa.

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kwa WANANDOA Wanaotaka Mafanikio Ya KIFEDHA…

i. Kukubaliana Falsafa Yenu Ya Pesa

ii. Kuwa na Maono ya Pamoja Kuhusu Pesa

iii. Kuweka Malengo Ya Pamoja Ya Kifamilia

iv. Kupanga Bajeti Ya Pamoja

v. Utaratibu Wa Msaada Kwa Ndugu

Katika Makala Hii Tutazungumzia Mbinu ya Pili.

– Kuwa na Maono ya Pamoja Kuhusu Pesa

Hapa kama wanandoa mnatakiwa mkae chini na mjiulize, hivi sisi maono yetu kuhusu pesa ni yapi?

Ni hatari sana pale ambapo mmoja wenu anataka kuwa tajiri sana wakati mwingine anasema “Mimi nataka maisha ya kawaida tu”.

Kumbuka hamuwezi kufanya mambo makubwa kwenye maisha kama hamjaoanisha maono yenu.

Maono yenu kuhusu pesa yanahusisha picha yenu kubwa ya Maisha ambayo mnataka kuyaishi huko mbeleni.

Kwa mfano:

• Mngependa kuja kuishi nyumba ya namna gani, ya fahari kubwa au ya kawaida tu?

• Mngependa kuwa mnaenda likizo wapi?

• Mngependa kuwa na uwekezaji wa kiwango gani?

• Mngependa kuendesha gari la aina gani mtakapofanikiwa kifedha?

• Mngependa kuwa mnaingiza kiasi gani katika uzee wenu hata bila kulazimika kuendelea kufanya kazi?

Yapitieni maswali haya kama sehemu muhimu ya kujenga maono yenu ya pamoja kuhusu pesa.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment