Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Umoja wa Ulaya, umeamua kuendeleza shinikizo ilizoiwekea Burundi mwaka 2015 hadi mwaka 2025.

Ripoti zinasema, Baraza la Umoja wa Ulaya, limetangaza kuongeza muda wa vikwazo hivyo hadi tarehe 31 mwezi Oktoba mwaka 2025.
Vikwazo hivyo, viliwekewa serikali ya Burundi, wakati huo ikiongozwa na Marehemu Pierre Nkurunziza, kutokana na rekodi mbaya ya haki za binadamu na kuwahangaisha wanasiasa wa upinzani na wanaharakati.
Wakati wa uongozi wa Nkurunzinza, aliifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo na kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu, na kuzua sintofahamu ya kisiasa nchini humo.
Kutoka na thathmini ya Umoja huo wa Ulaya, imebainika kuwa hali ya haki za binadamu imeendelea kuwa mbaya na hakuna mageuzi makubwa ya kisiasa yaliyofanywa na uongozi wa kisasa ili kuondoa vikwazo hivyo.

Aidha, Baraza la EU limesema, serikali ya Burundi inapaswa kuanzisha mazungumzo ya ndani ili kurejesha demokrasia thabiti nchini humo.
Miongoni mwa vikwazo ilivyowekewa ni pamoja na kuwazuia kusafiri maafisa wa serikali wanaodaiwa kuhusika na ukiukwaji wa haki za binadamu, mali zao zimezuiwa na Umoja wa Ulaya, Umoja huo pia umezuia misaada kwa serikali ya Burundi ambayo haijajibu kuongezwa muda kwa vikwazo hivyo.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.