Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Idadi ya watu waliofariki kutokana na mkasa wa ajali ya moto ya lori la kubeba mafuta imefikia watu 147.
Wengi wa waliofariki ni raia waliokimbia eneo la ajali kujizolea mafuta, baada ya lori hilo la mafuta kuanguka, kwa mujibu wa taarifa ya polisi, umati mkubwa wa watu ulifika kwenye eneo la mkasa kuyachota mafuta.
Lawal Shiisu Adam, msemaji wa polisi nchini Nigeria amesema watu wengine 100 wapo katika hali mahututi katika hospitali mbalimbali mjini Ringim, kwenye jimbo la Jigawa.
Dereva wa lori hilo hata hivyo hakuathirika na amekamatwa na polisi.

Visa vya ajali za moto kutokana na malori ya kubeba mafuta nchini Nigeria vimekuwa vikiongozeka kutoka na kile kinahusishwa na hali mbaya ya barabara na magari mabovu.
Mwezi ulliopita watu wengine 59 walifariki kutokana na mkasa wa moto baada ya lori la kubeba mafuta kugongana na basi la abiria.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.