Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://liveonlineradio.net/radio-fortune-africa
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji, IOM, limesema watu 45 wamekufa na wengine kadhaa hawajulikani walipo baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika pwani ya bahari ya Djibouti.

Kwa mujibu wa shirika hilo, boti hiyo iliyotokea Yemen ilikuwa na wahamiaji zaidi ya 300, ambapo mpaka sasa watu 32 pekee ndio wamefanikiwa kuokolewa wakati huu pia operesheni ya uokoaji ikiendelea.
Tukio hili kwenye pwani ya Djibouti, linajiri siku chache kupita tangu wahamiaji 12 wapoteze maisha katika pwani ya nchi ya Tunisia, baada ya boti kuzama wakijaribu kuelekea Ulaya kupitia bahari ya Mediterania.
Soma piaWahamiaji haramu tisa wafariki baada ya boti lao kuzama katika Visiwa vya #canary
Katika hatua nyingine, tume ya haki za binadamu ya umoja wa Mataifa, imesema nchi ya Tunisia imerudi nyuma katika ulinzi wa haki za wahamiaji, wakati huu dazeni ya wanaharakati wa haki za binadamu wakikamatwa.
Nchi ya Tunisia na jirani yake Libya, zimekuwa njia kuu za wahamiaji wanaojaribu kuelekea barani Ulaya.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.