Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://liveonlineradio.net/radio-fortune-africa
Muhtasari
- Abiria 100 hawajulikani walipo kufuatia ajali ya boti Nigeria
- Hezbollah yatangaza kukabiliana upya na wanajeshi wa Israel
- Israel yampiga marufuku katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo
- Iran: Khamenei azisuta nchi za magharibi baada ya kuishambulia Israel
- Jeshi la Sudan laapa kuendelea kupigana licha ya juhudi za amani
- Roketi takriban 100 zimerushwa kaskazini mwa Israel leo asubuhi
- Israel yatuma wanajeshi zaidi katika operesheni ya ardhini ya Lebanon
- Sean ‘Diddy’ Combs akabiliwa na madai mapya zaidi ya 100 ya unyanyasaji
- Mvutano unazidi kuongezeka Mashariki ya Kati huku mashambulizi yakiendelea
- Bei ya mafuta yapanda baada ya shambulizi la Iran
- Iran yanasema inaweza kuishambulia “miundombinu yote ya Israeli” ikiwa Israeli italipiza kisasi
- Tazama: Video inayoonyesha mashambulizi ya makombora ya Iran nchini Israel
- Marekani yasema iliisaidia Israel kuyadungua makombora ya Iran
- Netanyahu asema Iran italipia mashambulizi ya makombora, huku Israel ikianzisha mashambulizi mapya Beirut

Naibu wa Rais Rigathi Gachagua
Wandani wa Rais wa Kenya William Ruto waliwasilisha hoja bungeni siku ya Jumanne ya kumshtaki Naibu Rais Rigathi Gachagua wakimtuhumu kwa kuchochea chuki za kikabila na kuidhoofisha serikali.
Tofauti kati ya rais Ruto na Gachagua zimeongezeka katika siku za hivi karibuni. Gachagua anasema ametengwa na amekanusha shutuma za washirika wa Ruto kwamba alihusika na maandamano ya kupinga serikali mapema mwaka huu.
Pia wanadai kwamba Gachagua amejihusisha na masuala ya ufisadi , kuihujumu serikali na kukukuza siasa za kikabila.
Raia Ruto alimchagua Gachagua kama naibu wake katika uchaguzi wa 2022 ambapo walimshinda aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga katika uchaguzi wa urais uliokuwa na ushindani mkali.
Gachagua anatoka katika eneo la Mlima Kenya ambapo Rais Ruto alijipatia wingi wa kura ili kuibuka mshindi.
Tayari washirika wa kiongozi huyo wamefanya majaribio kadhaa ya kuzuia kura hiyo ya kutokuwa na imani naye bungeni.
Wabunge wanaomuunga mkono rais Ruto wamesema kwamba wana zaidi ya idadi inayohitajika ya kumuondoa kiongozi huyo serikalini.
Zaidi ya wabunge 250 wanadaiwa kuunga mkono hoja hiyo ya kumtimua naibu huyo wa rais madarakani.
Lakini ni kesi gani haswa inayomuandama naibu huyo wa rais bungeni?
Kulingana na mbunge wa Kibwezi Magharibi, Mutuse Mwengi, anakabiliwa na tuhuma kumi.
Gachagua analaumiwa kwa kukinzana na sera za serikali na kukosa kutekeleza majukumu yake kama Naibu Rais, hivyo basi kukiuka kanuni ya uwajibikaji wa pamoja wa Baraza la Mawaziri.
Hoja hiyo ya Mutuse Mwengi pia inadai kuwa Gachagua aliingilia shughuli za ugatuzi wa kaunti, kuhujumu ugatuzi na kutishia idara ya mahakama, hatua inayokiuka kanuni ya uhuru wa idara ya mahakama.
Vilevile hoja hiyo inataja utovu wa nidhamu, ikiwa ni pamoja na mashambulizi dhidi ya Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi, kutomtii Rais, kuwaonea maafisa wa umma, na kushawishi vitendo vya rushwa.
Mbunge huyo wa Kibwezi Magharibi anasema kwamba bwana Gachagua alishindwa kuheshimu na kutetea Katiba, huku matamshi yake ya uchochezi yakidaiwa kukiuka Sheria ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa kwa kuendeleza chuki za kikabila.
Aidha Gachagua anadaiwa alijihusisha na ufisadi, ufujaji wa pesa na matumizi mabaya ya ofisi, kukiuka sheria za kupambana na ufisadi , kutoa taarifa za uongo na uovu na kukiuka kanuni za adhabu na sheria ya uongozi na uadilifu.
Kwa kura hiyo kupita , itahitaji thuluthi mbili za wabunge ambao wanashirikisha wabunge wa chama cha Raila Odinga cha ODM ambaye hivi karibuni ameonekana akishirikiana na Rais Ruto.

Je, mchakato wa kumuondoa naibu wa rais unasemaje?
Mbunge, akiungwa mkono na angalau theluthi moja ya wajumbe wote, anaweza kutoa hoja ya kushtakiwa kwa naibu rais kwa msingi wa ukiukwaji mkubwa wa kifungu cha Katiba au sheria nyingine yoyote:
Pale ambapo kuna sababu kubwa za kuamini kwamba kiongozi huyo ametenda uhalifu chini ya sheria ya kitaifa au kimataifa; au kwa utovu wa nidhamu uliokithiri.
Iwapo angalau theluthi mbili ya wajumbe wa Bunge wataunga mkono hoja hiyo
Spika wa Bunge atamjulisha Spika wa Seneti kuhusu azimio hilo ndani ya siku mbili:
Naibu Rais ataendelea kutekeleza majukumu ya afisi ya Naibu Rais akisubiri matokeo ya kesi ya mashtaka.
Ndani ya siku saba baada ya kupokea taarifa ya azimio kutoka kwa Spika wa Bunge-
Spika wa Seneti ataitisha mkutano wa Seneti ndani ya siku saba ili kusikiliza mashtaka dhidi ya Naibu Rais; na Seneti, kwa azimio, inaweza kuteua kamati maalum inayojumuisha wanachama kumi na moja kuchunguza suala hilo.
Kamati iliyoteuliwa kuchunguza suala hilo itaripoti kwa Seneti katika muda wa siku kumi iwapo itapata maelezo ya madai dhidi ya Naibu Rais kuwa yamethibitishwa.
Wanachama wa Kamati Maalum watakula Kiapo au Uthibitisho, kama Spika wa Seneti atakavyoagiza, wakiwasilisha kwamba watatekeleza majukumu yao kwa uaminifu na kwa bidii.
Je, naibu rais atapewa fursa ya kujitetea?
Naibu Rais atakuwa na haki ya kufika na kuwakilishwa mbele ya kamati maalum wakati wa uchunguzi wake.
Kamati Maalum inaweza kusikiliza uwakilishi wa mjumbe aliyetoa hoja katika Bunge na wajumbe wengine wa Bunge.
Ikiwa kamati maalum itaripoti kwamba maelezo ya tuhuma yoyote dhidi ya Naibu Rais hayajathibitishwa, mashauri mengine hayatachukuliwa chini ya Ibara ya 145 ya Katiba kuhusiana na madai hayo.
Iwapo imethibitishwa, bunge la Seneti, baada ya Naibu Rais kupata nafasi ya kusikilizwa, itapiga kura kuhusu mashtaka ya kumshtaki.
Seneti itapiga kura ya ‘ndiyo’ au ‘la’ kuhusu kila shtaka la kumshtaki).
Iwapo angalau thuluthi mbili ya wanachama wote wa Seneti watapiga kura kuunga mkono shtaka lolote la kumshtaki, Naibu Rais atakoma kushikilia wadhifa huo.
Ikiwa hayajathibitishwa, Naibu Rais ataendelea kushikilia wadhifa huo.
Israel yathibitisha kifo cha mwanajeshi wake wa kwanza tangu uvamizi wa Lebanon

Mwanajeshi wa kwanza wa Israel amethibitishwa kuuawa ndani ya Lebanon tangu uvamizi wa ardhini kuanza.
Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lilitangaza katika taarifa kwamba Kapteni Eitan Yitzhak Oster, 22, aliuawa ndani ya Lebanon siku ya Jumatano.
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 22 alikuwa katika kitengo cha Egoz, cha makomando maalumu wa vita vya ardhini, IDF inasema.
Awali IDF iliripoti kuwa “inapigana maeneo kadhaa” kusini mwa Lebanon.
“Jeshi la Wanahewa la Israeli, waliwatimua magaidi na kuharibu miundombinu ya kigaidi kwa mabomu yaliyoongozwa kwa usahihi na ushirikiano ya karibu.”
Taarifa hiyo inaongeza “zaidi ya miundombinu 150 ya ugaidi” imeharibiwa na katika mashambulizi ya hivi majuzi.
Abiria 100 hawajulikani walipo kufuatia ajali ya boti Nigeria
Mamlaka katika jimbo la Niger ya Kati nchini Nigeria wamesema takriban abiria 100 hawajulikani walipo baada ya ajali ya boti iliyotokea jana usiku kwenye mto Niger.
Boti hiyo ilikuwa safarini kutoka Mundi ikiwa na zaidi ya abiria 300, wengi wao wakiwa wanawake na watoto.
Ripoti za vyombo vya habari nchini humo zinasema takriban miili 60 ilipatikana baada ya ajali hiyo.
Abiria wengi walisemekana kuhudhuria tamasha la Waislamu, sherehe za Maulid huko Gbajibo.
Mkuu wa Shirika la Usimamizi wa Dharura wa Jimbo la Niger Abdullahi Baba Arah alisema katika taarifa kwamba mamlaka hiyo imeanza kufuatilia shughuli za utafutaji na uokoaji kwa kutumia watu wa kujitolea na wazamiaji wa ndani.
Bw. Baba Arah alisema kuwa mwitikio wa haraka kutoka kwa wafanyakazi wa kujitolea wa jamii umewezesha zaidi ya watu 150 kuokolewa kufikia sasa.
Alieleza kuwa shughuli ya uokoaji bado inaendelea ili kupata manusura zaidi.
Chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana. Hata hivyo matukio ya kupinduka kwa boti katika Mto Niger ni ya kawaida hasa msimu wa mvua ambao hufanya kiwango cha maji mtoni kupanda.Mshirikishe mwenzako, Abiria 100 hawajulikani walipo kufuatia ajali ya boti Nigeria
Hezbollah yasema mapigano ya leo ni ‘awamu ya kwanza’ ya vita
Msemaji wa Hezbollah anasema mapambano yao ya leo dhidi ya Jeshi la Ulinzi la Israel kusini mwa Lebanon ni sehemu ya “duru ya kwanza ya vita”.
“Vikosi vyetu na wapiganaji wamejiandaa kikamilifu kukabiliana na adui,” Mohammad Afif wa Hezbollah aliwaambia waandishi wa habari, kama alivyonukuliwa na mashirik aya habari ya Reuters na NBC.
Afif anaongeza kuwa kundi hilo la wanamgambo lina silaha za kutosha kwa makabiliano na IDF.
Hezbollah na IDF wote wanaripoti mapigano ya ardhini ndani ya Lebanon siku ya Jumatano.
Hezbollah imetangaza hatuao hiyo baada ya wanajeshi wa Israel “kuvamia” mji wa Maroun al-Ras nchini Lebanon.
Mji huo uko karibu kilomita mbili kutoka mpaka wa Israeli-Lebanon.
Kwa mujibu wa Hezbollah, wanajeshi wa Israel waliingia kutoka upande wa mashariki, na mapigano yanaendelea, ilisema saa moja iliyopita.
Haya ni makabiliano ya pili ya moja kwa moja na wanajeshi wa Israel ambayo Hezbollah imedai leo.
Hapo awali, kundi hilo lilisema limefanikiwa kuzima uvamizi wa Israel nchini Lebanon.
Israel yampiga marufuku katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo

Waziri wa mambo ya nje wa Israel anasema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ”Hana rususa” kuingia Israel na amepigwa marufuku nchini humo.
Israel Katz anasema uamuzi wake unafuatia hatua ya Guterres “kutolaani” shambulio la kombora la Iran dhidi ya Israel siku ya Jumanne.
Anamshutumu mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa kwa kuwa “mpinzani wa Israel” na kutoa “msaada kwa magaidi, wabakaji na wauaji.Guterres atakumbukwa kama doa katika historia ya Umoja wa Mataifa kwa vizazi vijavyo.”
Jana, mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa alilaani “kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati” na kutoa wito wa kusitishwa kwa mapigano.
Iran: Khamenei azisuta nchi za magharibi baada ya kuishambulia Israel

Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, leo amekutana na kundi la wataalamu mjini Tehran.
Aliilaumu “Marekani na baadhi ya nchi za Ulaya” ambazo “zinadai kuleta amani na utulivu Mashariki ya Kati,” kwa kuchochea mvutano wa kikanda na vita katika eneo hilo.
Alisema lazima “watokomee” kutoka eneo hilo ili nchi za Mashariki ya Kati ziweze kuishi kwa amani.
Alisema kuwa “anaomboleza” kifo cha Kiongozi wa Hezbollah Hassan Nasrallah, lakini hakuahirisha mkutano wake na wataalamukwa sababu maombolezo ya Iran ni nguvu ya “kuhuisha na kuendesha”.
Agizo la kurusha makombora huko Israel siku ya Jumanne lilitolewa na kiongozi mkuu wa nchi hiyo – ambaye bado yuko katika eneo salama, afisa mkuu wa Iran aliliambia shirika la habari la Reuters.
Jeshi la Sudan laapa kuendelea kupigana licha ya juhudi za amani

Jenerali wa ngazi ya juu wa Sudan amesema jeshi litaendelea na mashambulizi yake licha ya juhudi za kimataifa za kukomesha mapigano katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miezi 17.
“Mazungumzo ya amani yanaweza kuendelea, lakini jeshi halitasitisha shughuli zake kwa sababu ya hilo,” Msaidizi wa Kamanda Mkuu Luteni Jenerali Ibrahim Gabir aliiambia BBC.
Alikuwa akizungumza siku chache tu baada ya jeshi kuanzisha operesheni ya kuchukuwa udhibiti wa mji mkuu, Khartoum, kutoka kwa waasi wa RSF.
Pande hizo mbili zimekuwa zikipigana tangu Aprili mwaka jana, baada ya viongozi wao kufautiana kuhusu mustakabali wa nchi.
Mzozo huo umesababisha janga la kibinadamu huku zaidi ya nusu ya nchi ikikabiliwa na njaa na mamilioni ya watu kulazimika kuyahama makazi yao.
Roketi takriban 100 zarushwa kaskazini mwa Israel leo asubuhi

Ving’ora vya tahadhari kuhusu mashambulizi ya roketi vimesikika kaskazini mwa Israel asubuhi ya leo.
Vikosi vya Ulinzi vya Israel vilitoa tahadhari kwa jamii zinazozunguka mji wa Haifa na Magharibi mwa Galilaya, karibu na mpaka wa Israel na Lebanon.
Kiasi cha roketi 100 zimerushwa kaskazini mwa Israel kufikia sasa hivi, vyombo vya habari vya Israel vinaripoti, vikinukuu Jeshi la ulinzi la Israel (IDF).
Awali Jeshi la Ulinzi la Israel lilitoa tahadhari mpya kwa watu wanaoishi katika vijiji karibu vijiji 25 vya kusini mwa Lebanon wahame.
Tahadhari hii inafuatia nyingine iliyotolewa jana kwa idadi sawa ya maeneo – takriban vijiji vitano vilivyojumuishwa katika ujumbe wa hivi punde pia vilijumuishwa kwenye tahadhari ya jana.
Tahadhari hiyo kutoka kwa msemaji wa Kiarabu wa IDF Avichay Adraee, lililowekwa kwenye mitandao ya kijamii, na linakuja baada ya ripoti za mapigano kusini mwa Lebanon.
Akiwahutubia wakazi wa Lebanon walioathirika, Adraee amesema jeshi la Israel halina nia ya kuwadhuru na wanapaswa kuhama mara moja hadi kaskazini mwa Mto Awali uliopo yapata kilomita 50 kutoka mpaka na Israeli – “kuokoa maisha yako. “
Mashambulizi ya Israel dhidi ya Beirut yanatia kiwewe – Mwanasiasa wa Lebanon

Baada ya usiku mwingine wa mashambulizi ya Israel dhidi ya Beirut, mwanasiasa wa Lebanon Michel Helou ameiambia BBC kuwa mji huo una “kiwewe”.
Mbali na majeruhi, mashambulizi hayo “yanaleta wasiwasi “, katibu mkuu wa chama huru cha National Bloc nchini Lebanon amekiambia kipindi cha BBC Newsday.
“Jana usiku hakuna hata mmoja wetu aliyelala sana kwasababu ilikuwa usiku wa tano mfululizo wa mashambulizi katika kitongoji cha kusini.
“Kila saa jeshi la Israel linatuma ujumbe wa Twitter ukiwaonya watu kuhama, lakini vipi na wapi na vipi inawezekana kwao kuhama katika muda wa nusu saa kabla ya shambulio kutokea.
“Bila shaka ni jambo linalosumbua sana kisaikolojia kwa binadamu kuwa katika mashambulizi hayo.”
Mjini Beirut, Israel imekuwa ikilenga kitongoji cha kusini cha Dahieh, ngome ya Hezbollah, na inasema inachukua hatua za kupunguza hatari ya kuwadhuru raia, ikiishutumu Hezbollah kwa kuficha miundombinu yake katikati ya raia.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.