Kipenga Cha Michezo-Tetesi za soka Ulaya Jumanne 01.10.2024

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://liveonlineradio.net/radio-fortune-africa

.

Mchezaji wa Inter Milan Simone Inzaghi na mkufunzi wa zamani wa England Gareth Southgate wanawania sana kuchukua nafasi ya meneja wa Manchester United iwapo klabu hiyo itamfukuza Erik ten Hag. (Daily Star)

Ruud van Nistelrooy pia atazingatiwa baada ya kurejea Manchester United kama kocha msaidizi msimu wa joto. (Times – Subscription Required),

Arsenal na Real Madrid ni miongoni mwa vilabu kadhaa vya Ulaya vinavyotaka kumsajili beki wa kati wa Palmeiras Vitor Reis, 18. (The Athletic – Subnscription Required)

.
Maelezo ya picha,Mason Greenwood

Barcelona wanatazamiwa kuwasilisha ombi la kumsajili Mason Greenwood wa Marseille – lakini wanakabiliwa na pambano kuu kutoka kwa Paris St-Germain kwa ajili ya kumnunua mshambuliaji huyo Mwingereza mwenye umri wa miaka 23. (Sun),

Real Madrid wako tayari kutoa ofa kwa kiungo wa kati wa Ufaransa Aurelien Tchouameni, 24, huku Liverpool ikiwa ni klabu inayopigania zaidi kufikia mkataba wa pauni milioni 66 msimu ujao. (Fichajes – In Spanish)

Aston Villa na West Ham wanapigania kumsajili mshambuliaji wa Valencia mwenye umri wa miaka 24 raia wa Uhispania Hugo Duro kwa hadi £25m. (Caught Offside)

.
Maelezo ya picha,Mario Balotteli

Mshambulizi wa zamani wa Manchester City na Liverpool Mario Balotelli, 34, yuko kwenye mazungumzo kuhusu kuhamia klabu ya daraja la tatu ya Uhispania Intercity. (AS – In Spanisha)

David Moyes angependa kurejea Everton ikiwa klabu hiyo itaachana na Sean Dyche baada ya kuanza kwa msimu. (Football Insider),

Jeraha la hivi punde la kiungo wa kati wa Manchester City Kevin de Bruyne halitaathiri mazungumzo ya kandarasi kati ya Mbelgiji huyo mwenye umri wa miaka 33 na timu hiyo ya Ligi ya Premia. (Football Insider),

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment