Unapofika kiwango cha mwisho cha maumivu.

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Ndio yuko kimya, Ila sio kwamba ana kiburi, la hasha…

Ni kwa sababu amefikia kiwango cha mwisho cha maumivu na hawezi kuongea tena.

Kuna watu tuko nao, marafiki, wenzi, watoto, wafanyakazi wenzetu n.k

Kuna wakati unawaona wako kimya, usihitimishe kuwa hawataki kuongea.

Kuna wengine, yaani nguvu zote zimewaishia kabisa na hawawezi hata kuongea kitu.

Kuna watu wanapitia maumivu ya mahusiano.

Wengine wamefanyiwa vitu ambavyo hawawezi kuviongea.

Wapo ambao wamesingiziwa na jamii imeshawahukumu n.k

Ukimuona unayempenda amekuwa kimya usiseme “Hataki kuongea”.

Inawezekana kuna maumivu yanamla ndani kwa ndani na amekosa kabisa msaada.

Kwa unayempenda, ukiona amekuwa kimya basi usimpuuze.

Tafuta namna ya kumsaidia.

Usimlazimishe aongee, unaweza kutengeneza mazingira tu ya kupata muda naye.

Mtoe “out”.

Mpe zawadi.

Mtafute mara kwa Mara kumsalimia n.k

Akijihakikishia kuwa unamjali sana, basi ataanza kufunguka.

Kama umeipenda makala hii…

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment