Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://radioslist.com/online/ke/fortuneafrica.html#infomore
Mashambulio ya Israeli nchini Lebanon yaliyolenga kundi la Hezbollah, yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 490 huku wengine zaidi ya 1500 wakijeruhiwa.
Haya ndio mauaji makubwa kuwahi kutokea kwa siku moja nchini Lebanon, baada ya miaka ishirini, ambayo pia yamesababisha maelfu ya watu kuyakimbia makaazi yao.
Jeshi la Israeli linasema, limeshambulia ngome 1,300 Hezbollah na kuharibu miundombinu ambayo kundi hilo linaloungwa mkono kundi la Hamas limekua likitumia tangu vita vya 2006. Daniel Hagari, ni msemaji wa Jeshi al Israel.
“Kwa zaidi ya miaka 20, Hezbollah imetuma wapiganaji wake ndani ya makazi, na kutumia miundombinu ya kiraia, kutokana na hilo, kundi hili la kigaidi limeigeuza eneo la Kusini mwa Lebabon kuwa uwanja wa mapambano.” AlisemaDaniel Hagari, msemaji wa Jeshi al Israel.

Katika hatua nyingine, Josep Borrel, mkuu wa será za kigeni wa umoja wa Ulaya amesema mzozo kati ya Israeli na Hezbollah unakaribia kuwa vita kamili.
“Kuendelea kwa mzozo huu ni hatari sana na unatia wasiwasi, naweza kusema kuwa tunakaribia kushuhudia vita kamili.” AmeelezaJosep Borrel, mkuu wa será za kigeni wa umoja wa Ulaya
Jumuiya ya kimataifa imeonekana kutilia shaka mashambulio ya Israeli nchini Lebanon, Marekani ikisema itatuma vikosi zaidi eneo la mashariki ya kati huku Ufaransa nayo ikiitisha kikao cha dharurua cha baraza la usalama la umoja wa mataifa kujadili mzozo huo.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.