Wanajeshi wa Israeli waripotiwa kurusha mabomu kuelekea kusini mwa Lebanon

Jeshi la Israeli limerusha mabomu Kusini mwa Lebanon, baada ya mashambulio kutokea kwenye vifaa vya mawasilino vilivyokuwa vinatumiwa na kundi la Hezbollah, na kusababisha maafa na majeruhi.

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Moshi ikionekana kaskazini mwa Israeli kufuatia kombora kutokana nchini Lebanon, Alhamis, Sept. 19, 2024. (AP Photo/Baz Ratner)
Moshi ikionekana kaskazini mwa Israeli kufuatia kombora kutokana nchini Lebanon, Alhamis, Sept. 19, 2024. (AP Photo/Baz Ratner) AP – Baz Ratner

Milipuko imesikika hadi katika jiji kuu Beirut, huku vyombo vya habari nchini Lebanon, vikiripoti kuwa ndege za kijeshi za Israeli zimeonekana zikipaa kwenye angaa la nchi yao katika maeneo ya mipaka.

Hatua hii ya jeshi la Israeli inakuja, baada ya Israeli kusema kuwa, inapambana na Hezbollah, kama inavyofanya dhidi ya Hamas kwenye ukanda wa Gaza.

Mbali na kilichoripotiwa kwenye mpaka wa Lebanon, jeshi la Israeli limeendelea kurusha mabomu kwenye ukanda wa Gaza, baada ya watu sita kuuawa kwenye nyumba moja.

Wanajeshi wa jeshi la Lebanon wakiwa karibu na gari la wagonjwa baada ya mlipuko kusini mwa Beirut, Septemba 18, 2024.
Wanajeshi wa jeshi la Lebanon wakiwa karibu na gari la wagonjwa baada ya mlipuko kusini mwa Beirut, Septemba 18, 2024. AFP – FADEL ITANI

Haya yanajiri saa chache tu, baada ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kwa kura nyingi, kupitisha azimio la kuitaka Israeli kumaliza vita kwenye ukanda wa Gaza na kuondoka kwenye ardhi ya Wapalaestina.

Katika hatua nyingine, vyombo vya Habari nchini Israeli vimeripoti kuwa, nchi hiyo imependekeza mkataba mpya, ili kuachiwa kwa mateka, mapendekezo ambayo yamewasilishwa kwa Marekani ambao ni wasuluhishi wakuu.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment