Jeshi la Marekani hapo jana limetangaza kukamilisha kuwaondoa wanajeshi wake wote nchini Niger, miezi michache kupita tangu utawala wa kijeshi wa Niamey usitishe ushirikiano wa kijeshi na Washington na kuagiza vikosi vyake kuondoka.
Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Marekani ilikuwa na wanajeshi elfu moja nchini Niger, ambao wamekuwa sehemu ya kikosi cha kupambana na wanajihadi katika ukanda wa Sahel lakini pia kambi ya operesheni za ndege zisizo na rubani.
Kamandi ya kijeshi ya Marekani barani Afrika, AFRICOM, imesema shughuli hiyo imemalizika salama na vikosi ikisifu ushirikiano wa awali uliowezesha kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Niger katika kukabiliana na wanajihadi.
Tangu kupinduliwa kwa rais Mohamed Bazoum, utawala wa kijeshi chini ya uongozi wa jenerali Abdourahmane Tchiani,umekuwa na uhusiano baridi na nchi za magharibi, ikiwemo Mkoloni wake wa zamani Ufaransa.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.