Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Kuna hali ngumu sana unaipitia leo na maumivu ni makali…
…maswali ni mengi sana unajiuliza.
Dalili zote zinaonyesha umefika mwisho…
…na kila unakogeuka haupati msaada.
Ulipofika ni kama unajiambia “sina thamani tena…
…sitaweza kuinuka tena na hakuna faida ya kuishi tena”.
Ukitafakari hakuna ubishi kuwa sio rahisi kuinuka tena.
Unajiambia “kama ni kulia basi nimelia hadi machozi yameisha, kama kuomba nimeshaomba sana…
…kama ni kufanya bidii nimejaribu kila mbinu ila sijaona matokeo”.
Nimetumwa nikukumbushe yafuatayo:
1. Usijaribu kufikiri kuwa MUNGU amekuacha na hakujali tena:
Bado anakuwazia mema.
Ingawa wewe unayo njia nzuri, kumbuka yeye anaona zaidi yako…
…na anajua zaidi yako – Badala ya kulaumu endelea kumuamini.
2. Na hili nalo utashinda.
Kumbuka lile gumu ambalo ulipitia huko nyuma na uliona kama hautavuka lakini ulivuka…
…NA HILI NALO UTASHINDA na itabakia historia.
3. Usijifungie peke yako, usijitenge peke yako.
Kuna mawazo yanakuambia kila mtu hayuko tayari kukusaidia…
…hilo sio kweli na usiliamini.
Mungu bado anao watu wanaokuthamini, wanaokupenda…
…wanaokuwazia mema na wako tayari kukusaidia.
Hata kama wengi wameonekana hawako tayari kukusaidia BADO wapo ambao WANAKUTHAMINI na WATASIMAMA na wewe.
Toka ndani na kutana na watu,kuna mtu amendaliwa ila ili ukutane naye lazima utoke.
Nasubiria siku ambayo utaibuka mshindi na utakuwa umelivuka hili kwa ushindi. NAALO LITAPITA.
Naomba kama umejifunza kitu fanya mambo haya mawili…
All Rights Reserved @ Cantona Group PLC||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.