Urusi inasema wanajeshi wake wamechukua vijiji zaidi nchini Ukraine

Urusi inasema imechukua vijiji viwili zaidi mashariki mwa Ukraine haswa katika maeneo ya Donetsk na Lugansk ambapo wanajeshi wake wameendelea kuripotiwa kupiga hatua katika uwanja wa mapambano.

In this photo taken from video released by Russian Defense Ministry Press Service on Tuesday, June 18, 2024, a Russian soldier takes aim with an anti-drone gun at an unknown location in Donetsk region

Wizara ya ulinzi ya Urusi imeeleza kwamba maofisa wake wamechukua kijiji cha Mykolaivka, karibia kilomita 15 kutoka katika mji wa Pokrovsk katika jimbo la Donetsk, sawa na eneo lenye makazi ya watu ya Stelmakhivka, jirani na Lugansk.

Wanajeshi wa Urusi wamekuwa wakipiga hatua kuelekea katika mji wa kimkakati wa Pokrovsk, ambapo karibia watu Elfu 60 wamekuwa wakiishi katika miezi ya hivi karibuni.

Mwanajeshi wa Ukraine akielekea katika mji wa Lysychansk mashariki mwa Ukraine huko Donbass, Juni 9, 2022.

Wanajeshi wa Ukraine wameonekana kukabiliwa na upungufu wa silaha haswa wakati huu wanapoendelea kusubiria silaha kutoka katika nchi washirika wake.

Mapema mwezi huu, Kyiv ilianzisha mashambulio ya ardhini katika eneo la Kursk kwenye mpaka na Urusi ikiwa na matumaini ya kuwaondoa wanajeshi wa Urusi kutoka katika eneo la   Donetsk.

Wanajeshi wa Urusi wameendelea kuripotiwa kupiga hatua mashariki mwa Ukraine licha ya Kyiv nayo ikiendelea na mashambulio yake katika mji wa Kursk nchini Urusi.

Licha ya mashambulio ya Ukraine katika mji wa Kursk, Urusi katika upande mwengine imeonekana kuendelea kupiga hatua katika mji wa viwanda wa Donetsk.

Haya yanajiri wakati huu shambulio la Urusi katika mji wa Nikopol kusini mwa Ukraine likiripotiwa kusababisha kifo cha mtu mmoja, wengine watano wakiwa wamejeruhiwa kwa mujibu wa mamlaka.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC ||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment