Radio Fortune Africa
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Natumai u Buheri wa afya popote ulipo duniani,karibu julai ya 27 Katika awamu Afrika Mwisho Juma, Naitwa Cantona Joseph
INATOKEA SASA HIVI
SIKILIZA RADIO FORTUNE AFRICA
HABARI
Haiti: Makundi mawili yenye silaha yatia saini makubaliano ya kumaliza mvutano
Viongozi wa makundi mawili yenye silaha nchini Haiti wameripotiwa kutia saini makubaliano ya kumaliza mzozo.
Dakika 2

Na: Radio Fortune Africa
MATANGAZO YA KIBIASHARA
Haiti imekuwa ikikabiliwa na machufuko yanayotokana na makundi ya watu wenye silaha yanayowahangaisha raia, baadhi ya wangine wakitekwa.
Hali ilikuwa mbaya zaidi mwezi Februari baada ya watu wenye silaha kutekeleza shambulio katika mji mkuu wa Port-au-Prince wakiwa na nia ya kumtimua madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu wa wakati huo Ariel Henry.
Makundi yenye silaha yanaripotiwa kudhibiti sehemu kubwa ya taifa hilo ambapo yanatuhumiwa kwa kutekeleza mauaji, uporaji wa mali pamoja na utekaji wa raia ilikulipwa kikombozi.
Kwa mujibu wa makubaliano hayo kati ya viongozi wa kundi la G9 na lile na G-Pep, vizuizi vya barabarani katika mji wa shantytown wenye karibia watu laki tatu viliondolewa.
Mchungaji Jean Enock Joseph, mwenye umaarufu katika eneo hilo, ameeleza kwamba makubaliano kama hayo yaliafikiwa mwaka wa 2023 kabla ya kuvunjika majuma kadhaa baadae.
Kama ilivyo kwa raia wengi katika mji wa Port-au-Prince, wakazi wa Cite Soleil walikuwa wamezuiwa kutembea kwa uhuru katika mtaa wa mabanda uliogawanywa katika mitaa zinazodhibitiwa na magenge hasimu kwa hofu ya kuathiriwa kwenye makabiliano.
Magenge ya G9 na G-Pep hayajaripotiwa kuingia katika makabiliano tangu Februari, walipojiunga na muungano ulioanzisha kumpindua Henry.
Jimmy “Barbecue” Cherizier, mkuu wa G9 na mmoja wa viongozi wa muungano huo, alisifu ujasiri wa viongozi wa genge la Cite Soleil siku ya Alhamisi.
Ghasia katika mji wa Port-au-Prince zimeongezeka katika miezi ya hivi karibuni, na kuzua mzozo mkubwa wa kibinadamu.

Takriban watu 600,000 wamekimbia makazi yao nchini Haiti, kulingana na Umoja wa Mataifa, ongezeko la asilimia 60 tangu Machi.
Tangu kuondoka kwa Ariel Henry, mamlaka za mpito zimeundwa ili kuirejesha utulivu na uongozi thabiti kwenye taifa hilo.
Kenya inaoongoza kikosi cha polisi wa kimataifa kujaribu kurejesha hali ya utulivu nchini Haiti
Soma zaidi mada inayofanana:
Habari zinazofanana

Barack Obama atangaza kumuunga mkono Kamala Harris katika uteuzi wa chama cha Democratic

Haiti: Makundi mawili yenye silaha yatia saini makubaliano ya kumaliza mvutano

Brazil: Brazil yarekodi vifo viwili vilivyotokana na Oropouche
Marekani: Trump akataa mdahalo wowote na Kamala Harris kabla ya kuteuliwa rasmi na Democrats

Marekani yatangaza kukamatwa kwa ‘El Mayo’ na Guzman, viongozi wawili wa kundi la Sinaloa
Marekani: Kamala Harris aahidi “kutokaa kimya” kuhusu Gaza baada ya mazungumzo na Netanyahu
Joe Biden ampokea Benjamin Netanyahu ili kujaribu kuendeleza mazungumzo kuhusu Gaza

Biden anaelezea kujiondoa kwake kwa hitaji la ‘kuunganisha’ chama chake na ‘kukabidhi mwenge’

Benjamin Netanyahu aapa kuendelea na vita Gaza mbele ya Bunge la Marekani lililogawanyika

Marekani: Kamala Harris kufafanua msimamo wake ili kuvutia wanaounga mkono Palestina
Mkurugenzi wa Huduma ya Secret Service ajiuzulu kufuatia jaribio la kumuua Trump

Marekani: Kamala Harris ajivunia kuwa na uungwaji mkono wa kutosha ili kuteuliwa kuwa mgombea
Marekani: Kamala Harris, amepata uungwaji mkono kutoka kwa chama cha DeMOCRATS
WIMBI LA SIASA MAREKANI
Makala haya yanatupia jicho uchaguzi wa urais nchini Marekani, nini maana ya ushindi wa Makamu Rais Kamala Harris
AFRIKA YA MASHARIKI
Nishati inachangia asilimia kubwa kwa ukuaji wa Uchumi wa mataifa.
UCHUMI NA BIASHARA
Kuberoshwa kwa huduma ya intaneti Kenya na ilivyochochea ubora.
SANAA YA AFRIKA
Ambwene Mwasongwe Muimbaji wa Nyimbo za Injili kutoka nchini Tanzania asimulia Safari yake ya Sanaa ya nyimbo za kumwabudu Mungu,anavyotunga nyimbo Katika uhalisia wa matukio ya kila siku maishani,mfano hai ni katika wimbi wake majaribu ni Mtaji.
All Rights Reserved © Cantona Group Ltd||2024
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.