Je nani ameshikilia furaha yako.

Radio Fortune Africa -Bao la Asubui

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na Cantona Joseph

Unakosa furaha katika maisha yako? Nani ameshikilia furaha yako…

Moja ya kitu hatari sana kwenye maisha yako ni…

…kuruhusu FURAHA yako ishikiliwe na KITU au MTU.

Kuna watu wameruhusu maisha yao yawe kama TV.

Yaani kuna mtu ana “Remote Control” mahali…

…ndiye ambaye anaamua kila kitu kuhusiana na MAISHA yao.

Yaani, anaweza kuamua WACHEKE MUDA GANI

Au WANUNE MUDA GANI.

Ameshajua akitaka kuwafanya siku yao iharibike awafanyie/kuwaambia nini.

Ukiwa mtu ambaye FURAHA yako inashikiliwa na mtu mwingine…

…ina maanisha MAISHA yako yameshikiliwa na huyo mtu.

Fanya maamuzi kuwa Furaha yako ni Jukumu lako.

La sivyo, kuna siku huyo anayeshikilia furaha yako atafanya kitu…

…na utajiona kama haustahili KUISHI TENA.

Usiruhusu furaha yako ISHIKILIWE NA MTU MWINGINE!.

Natumai makala hii imekusaidia.

Kama imekusaidia na umeipenda na unataka ujifunze zaidi…

Uweze kupata mbinu zilizowasaidia mamia ya watu kuweza kutimiza malengo yao kwa kasi kubwa sana.

Na Hili ndilo bao la Asubui -salamu ziwafikie wakaazi wa banana kiambu Nchini Kenya.

All Rights Reserved © Cantona Group Ltd||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment