“Nani ataniambia Ukweli Ili Nisiangamie?”
Kuna wakati kwenye maisha, USALAMA wako…
…uko mikononi mwa watu wenye UJASIRI wa kukuambia ukweli ili USIANGAMIE.
Kuna watu wengi ambao wanapata nafasi ya kuwa KARIBU na sisi…
…Ila wanajua wakituambia TUSICHOPENDA kusikia au KINACHOUMIZA basi wao watapoteza FURSA.
Hii ndio maana unaweza kushangaa, watu wa karibu ya mtu wenye UWEZO wa kushauri VIZURI…
…ndio wanaoongoza KUPOTOSHA.
Cha ajabu ni kuwa, siku aliyepotoshwa AKIHARIBIKIWA…
…wale waliompotosha WANAHAMIA kwa MWINGINE.
Mfalme wa Israel alikuwa anamchukia mtu mmoja (MIKAYA)…
…ambaye alikuwa HAOGOPI kumwambia ukweli.
Siku moja, mfalme ALIWAITA watu 400 kuwaomba USHAURI…
…na wote wakamwambia UONGO ili WAMFURAHISHE.
Mikaya peke yake ndiye alisema UKWELI.
Alipouchukia UKWELI wa Mikaya…
…ndio ilikuwa CHANZO cha ANGUKO na KIFO chake.
Tusiwafurahie WENGI wanaotuambia tunayopenda kuyasikia…
…tumpe nafasi “MIKAYA” ili atuambie KILICHO SAHIHI PIA.
Usisahau wenye UWEZO wa kukuambia UKWELI ni wachache…
…na huwa HAWAFANYI BIDII kuongea na wewe, inatakiwa UWAPE KIPAUMBELE.
Mpe nafasi MIKAYA pia Aongee, Itakuokoa na HATARI!
Kama umejifunza kitu comment maneno “NIMEJIFUNZA KITU”.
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.