Chagua kunyamaza….

MITHALI 11:
12 Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

MITHALI 17:
28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima;Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu

Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa

Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu

Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu

Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu

MUHUBIRI 3:
1 Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

Ipo nguvu katika kunyamaza

Yapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwaajili ya usalama wa Roho zetu

Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lkn ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani

Unajua ni kwanini?

Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafirika, moyo ukighafirika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu

Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima

Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho

Sasa jiulize majibu yanayotoka kutokana na msukumo wa hasira huwa yanakuwaje? Mazuri? Ya upole? Ya hekima? Ya unyenyekevu? I am sure jibu ni hapana

Kama jibu ni hapana that means utaongea vitu vibaya ambavyo ni chukizo kwa MUNGU-kaa kimyaaa

Sasa badala ya kuongea upumbavu na ukamkosea MUNGU kwanini usichague kunyamaza?

AMOSI 5:
3 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya

Nimekuwa inspired sana na mwanamke Abigaili, ni kweli mumewe alikuwa na makosa, ni kweli alikuwa mlevi, lakini mwanamke huyu alijua ni wakati gani, na mazingira gani alipaswa kuongea na mumewe na alijua aongee nini. Alipomkuta mumewe yupo katika hali ya ulevi, ALINYAMAZA, alijua kuwa huu sio wakati wa kusema jambo lolote

1 SAMWELI 25:1

Ni vyema sisi pia tukajifunza kusoma mazingira na nyakati na hali za watu zilivyo ili tujue ni wakati gani tujibu, tuongee nini na ni wakati gani tunyamaze

Kilinde kinywa, hakikisha haukiachi kinene mabaya – ZABURI 50:19

Usipoteze marafiki na kuharibu mahusiano kwaajili ya kibovu – MITHALI 11:9

Ni vyema tukajifunza kujua ni neno gani tukitamka kwa wakati/hali/mazingira gani litakubaliwa –MITHALI 10:32

ZABURI 19:14 – Bwana na akafanye maneno yetu yakapate kibali mbele zake MUNGU na mbele za wanadamu pia

1SAMWELI 25:36

Umeumizwa, umekwazwa, umetukanwa, umedharauliwa, KATIKA MAZINGIRA YA HASIRA NA GHADHABU JITAHIDI KUNYAMAZA

Ni kweli moyo na akili na hisia vinakusukuma kujibu, kubisha nk nk lakini elewa impact za kujibizana ukiwa na hasira na hizo zikufanye ukae kimya.


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment