Usilie tena mpendwa wangu jivike nguvu kwa upya,

Niko hapa kukutia moyo kuwa kuvuka ni lazima haijalishi umekwama kwenye eneo lipi amini kuwa kuvuka ni lazima

Kuna wakati katika maisha,yoote uliyoyategemea hayaonekani kama yatatokea na woote uliowategemea wamekukimbia katika mazingira na kipindi usichotazamia

Katika kipindi cha namna hii unaweza kuwa na kitanda kizuri lakini kisikupe usingizi kwasababu ya maumivu ya moyo kutokana na mambo uliyokutana nayo ambayo hukuyategemea

Najua naongea na mtu hakuna kinachoonekana kukupa tumaini kwenye maisha yako na umefika mahali moyoni una maumivu na uchungu usioelezeka

Ile furaha ya maisha imepotea gafla kama mshumaa,na zile nguvu za kuendelea mbele gafla zimepotea ndani ya mifupa yako hujisikii tena kuendelea na chochote

Na ule mwanga uliokuwa unauona gafla umezimika na giza nene limetanda mbele yako huoni tena pakupita,mawimbi ni mengi sana yaliyotanda mbele yako

Hata Mungu uliyemtegemea kwamba angekusaidia ni kama na yeye amenyemanza gafla umejikuta huna tena msaada,moyo wako umejawa na wasiwasi hujui msaada utatokea wapi tena

Nikiwa katika maombi nikasikia roho mtakatifu akiniambia mtie moyo huyu dada mwambie safari yako haiwezi kuishia hapa

Nikasikia tena sauti ikiniambia mtie moyo huyu mama mwambie ndoa yako haiwezi kufia hapa bado lipo tumaini

Nikasikia tena sauti ikiniambia mtie moyo huyu Baba mwambie akili za mwanadamu zinapoishia ndipo Mungu anapoanzia atafanya

Mpendwa ninakuombea mpaka uvuke ng’ambo na ninakuhakikishia ya kwamba yeye aliyewavusha wana wa Israel wakavuka ng’ambo ya bahari ya shamu atakuvusha na wewe pia hatakuacha

Usilie tena mpendwa wangu jivike nguvu kwa upya, anza tena,jaribu tena utavuka ng’ambo.


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment