Nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,Sitaogopa mabaya;Kwa maana Wewe upo pamoja nami,Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
Moja kati ya jambo unalohitaji kulijua ni hili kwamba nyakati ngumu unazozipitia kimaisha ziwe ni za kiuchumi,kiafya au kimahusiano huwa hazidumu katika maisha
Kumbuka, kama kuna usiku kuna mchana pia,kama kuna mwanzo kuna mwisho pia,hakuna lenye mwanzo ambalo halina mwisho
Ninajua mahali Dunia inapita matumaini ya wengi yamepotea,ndoto za wengi zinazimika kama mshumaa,mipango ya wengi inakufa mioyo ya wengi imeugua kwa hofu
Ninakutia moyo wewe unaesoma ujumbe huu, nyakati ngumu huwa hazidumu kwenye maisha hata huu wakati utapita pia Amini tu katika bonde la uvuli wa mauti sio mahali Pakukaa ni mahali tunapita tu
Ninakuombea siku ya leo Mungu ninaemtumikia akutetee na akutoe katika hilo bonde la uvuli wa mauti na ukamuone Bwana katika jina la Yesu
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.