Unapopitia katika njia ngumu.

Mungu atakupitisha kwenye njia ngumu na hatari wakati mwingine njia zenye majonzi na hofu njia ambazo mwanadamu wa kawaida hawezi jaribu kutamani kupita lkn mwisho wa hatari ni Amani isiyo na kifani,mwisho wa uwoga anakupa ujasiri utasahau majonzi atakupa furaha isiyo kuwa na kipimo hiyo ndiyo tabia ya Mungu.

Pale ambapo watu wamefikia mwisho kufikiri ndipo Mungu huanzia hapo.Unaezani kwamba umefikia ukomo Mungu ndio anataka kuanza hapo.Ni maombi yangu leo Mungu akakuinue na kukutoa hapo ulipo kwama na akuvushe kwa mkono wake wenye nguvu

Kila jambo na wakati wake,kila wakati una maana sana na kusudi lake.Kama ulikua unalia kuna furaha inakuja mbele yako,kama ulionewa na kudharauliwa heshima inakuja kwako,waliokupiga vita sana mwaka jana mwaka huu ni majira ya amani na furaha kwako.

(Mhubiri 3;1) Huu ni wakati uliokubalika na wote wenye imani watapokea miujiza mikubwa kwa Jina la Yesu.
Kilichofanya wakina Mariam na Magdalena kuendelea kwenda kaburini alipo lala Yesu baada ya kufa wakiwa na manukato na manemane na uvumba sio tu upendo bali walillishika neno kama alivyosema Yesu kabla ya kufa atasurubiwa na kufa lkn siku ya 3 atafufuka,kwaio walikua wanafanya hayo yote wakiamini atakuwa hai tena baada ya siku ya tatu.

Hata wewe kuwa na imani na neno la Mungu na kulishika,Yesu akasema ndugu zake ni wale wanaolishika neno la Mungu na kulitii.Mungu anakwenda kujibu maombi na hitaji lako kabla ya mwaka kuisha amini neno hili katika Jina la Yesu.

CantonaJoseph’s contacts

Facebook https://www.facebook.com/CantonaJoseph/

Instagram https://www.instagram.com/Cantona.Joseph.

Twitter https://twitter.com/@CantonaJoseph

LinkedIn https://www.linkedin.com/in/CantonaJo

Management Fortune Baraka Entertainments

Website https://CantonaJoseph.Wordpress.Com

Email:fortunebaraka.entertainmentsltd@gmail.com

cantona.online254@gmail.com

Contacts +254748836127

Wewe ni wa maana sana!

All Rights Reserved @2020/FortuneBarakaEntertainments.


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment