Mateso uliyonayo yataondoka ukimkiri Yesu kuwa Bwana.Utaokolewa

WAKIAMBIWA HABARI ZA MUNGU NA NGUVU ZAKE, WATAMKIMBILIA WAPATE KUOKOLEWA

MAANA WALIPO NA WALIVYO, WAMEKANDAMIZWA BARA-BARA NA NGUVU ZA SHETANI

Fikiria watoto wa shule za msingi, sekondari,wanaanguka ghafla siku za kukaribia mtihani au hapa na pale katika majira fulani ya mwaka

Fikiria watoto wadogo shule ya msingi,baadhi wametekwa nyara na waganga, walozi,wachawi konki na konkodi.

Maana walishatolewa kafara kwa mizimu na kufundishwa, shirikishwa, husishwa na uchawi na tubibi twao wakiwa bado chalii kabisa

Fikiria kila ujauzito unatoka na wakizaliwa hawavuki miaka 5 wanakufa

Fikiria ukoo wao wote, wanawake hawaolewagi na ikitokea wameolewa, wanaachika,ndoa hazidumu.

Fikiria ukoo wao,wasichana wanazalishwa wakiwa shuleni, hakuna anayevuka kwenda chuo na chuo kikuu

Fikiria kuanzia babu na bibi ni wavuta bangi, tumbaku na ugolo mpaka baba na mama na watoto kwa kwenda mbele

Fikiria ukoo ambao wao kujiua na kuua ni kitu cha kawaida kama kusukuma bembeya na kubembea

Fikiria wanabeba mimba wakati wa kuzaa wanazaa mifuko ya rambo na kokwa za embe na maparachichi.

Fikiria mtu analewa mpaka kujikojolea, kulala mtaroni au wale wanaotumia madawa ya kulevya na kuanza kubembea njiani

SWALI: Watatokaje kwa hayo madubwasha wanadamu hao?

SWALI: Nani, atawaokoa jibu? ni Serikali, Jamii, mashirika yasiyo ya serikari ?

Imeandikwa:

Wakolosai. 1: 13 Naye alituokoa kutoka ufalme wa nguvu za giza,akatuhamisha na kutuingiza katika Ufalme wa mwana wa pendo lake

Ni Injili pekee-habari za wokovu wa Yesu Kristo ndiyo nguvu ya kuwang’oa kwa hayo

Kila mteule, popote mlipo, hubirini Injili hapana kabisa mchezo, hubiri Injili, na jina la Yesu lisifiwe kote.Simama katika pengo kuiombea jamii iliyotekwa nyara.

Ungana nasi kufikisha injili mbali.


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment