USIWE MWEPESI KUTOA TAARIFA

Watu wengi wameumizwa na marafiki, vyombo vwa habari, maadui, shetani, au na watu waliowaamini sana, sababu kubwa ikiwa Kutojua madhara ya taarifa ambayo wameitoa wakidhani wanasaidia wasijue hiyo taarifa inaumiza au itatoa maadhara ni silaha kali,ni upangak wa kuharibu na kuwaumiza wengine.
Shetani alipokuja kwa Hawa aliuliza taarifa ya pili ambayo ama hakuijua au hakuwa na uhakika nayo ila alitaka ushahidi wa muhusika mwenyewe ili apate njia ya kumuumiza na akafanikiwa na kuleta majanga ambayo mpaka leo tunayalipia.
Soma hii Mwanzo 3:1-6
Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?… endelea kusoma majibu ya mwanamke… Mwanamke akampa taarifa na akadanganywa kwa ushauri ambao haukufaa.
Haijalishi umefanya nini,liwe nzuri au baya maadamu adui yako,rafiki yako,mtu unayemwamini,hata taarifa ya pili ambayo ukweli wake ni wewe pekee yake unaujua. Tafadhali usijaribu kumpa hiyo taarifa,ukidhani kwa kumpa unajitetea,utaeleweka,utajisafisha,ama atakupa uhalali fulani.


Akaonyesha kuitafuta kaa nayo, kwa nini ije ikuumize zaidi? haijalishi unasemwa nini upo ukweli unaoujua wewe, haijalishi unasifiwa ama kuchukiwa upo ukweli unaoujua akitokea mtu anatafuta uhakika wa ukweli huo jihadhari sana USIMPE.
Bora wewe ukaomba ushauri kwa mtu unayemwamini kuwa anaweza kukupa suluhu, kuliko mtu unayedhani anafaa kuitafuta kwa nguvu taarifa yako ya pili ya kilichotokea mwanzo ama kizuri ama kibaya.Nakuonya Tena usimpe taarifa ya pilu,kaa nayo koyoni maana haiui,Hata Kama inauma,inatokota inawasha,inauma,inatokota,inawasha,inatoa Moshi,jikaze usiitoe,muda utakusaidia kuishinda Hali hiyo.Nyamaza nayo kimya Mungu atakupa mlango was kutokea.

#Iposiku #GetInspired #CantonaJosephMotivates. #CantonaJoseph’sWorld. #CantonaJosephIntMinistries. #TwapigaHatuaPamoja.

Allrights reserved ©2019


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment