Usitoe kafara,ili upate nguvu za kiroho,Mungu huchukia hilo.

Watu hutoa kafara ili kupata nguvu za kiroho,na kwa njia hiyo kweli wanapata nguvu sawa sawa na neno kutoka Waebrania 9;13 lakini neno linasema anaewafanyia kafara yaani mganga naye ni mchafu ndio maana nguvu pia zinapatikana ambazo ni za giza hazina nuru.Yesu alikuja kukomboa ulimwengu kwanza akafundisha ili watu wajue kwanini amekuja kisha akafanya miujiza akaponya na kuwaweka watu huru ili watu waamini Mungu ana uwezo mkubwa kwakua walizoe kusimuliwa habari za mababu zao kwamba Mungu aliwahi pasua mpaka bahari ya shamu,baada ya hayo yote Yesu akasurubiwa na akafa pale msalabani alijitoa kafara lakini kafara yake ni tofauti yeye ni mwana wa Mungu hakua na dhambi kafara yake ilikua ni kwaajiri ya ukombozi wa dunia nzima,na yeye si mchafu (Waebrania 9:13-14) hauna haja tena ya kufanyiwa matambiko na kutoa mbuzi kuku au ng’ombe Yesu alikwisha kukomboa.Ukisikia habari kwamba umefanyiwa tambiko wakazika kuku kichwa chini miguu juu wala usiogope jua Yuko aliyemkuu mwenye thamani mtoto wa Mungu alikuja duniani yeye akakubali kufa awe kafara juu yako akapigwa na kuchomwa mkuki ubavuni ile damu iliyo mwagika ndio ilikufanya ukawa huru.
#Iposiku #Getinspired #CantonaJosephMotivates

Alrights reserved©2019


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment